Video Information
TAARIFA YA
HABARI MARCH,4,2016.
KWANZA MUKHTASARI WAKE.
- Jeshi la polisi mkoani
Kilimanjaro,linamshikilia mkazi wa kijiji cha Kisangesangeni,wilayani Moshi
vijijini,Aboukar Macha,kwa tuhuma za kumiliki silaha kinyume cha sheria.
- Mamlaka ya Udhibiti
na Usimamizi Usafiri wa Majini na Nchi Kavu,SUMATRA, mkoani
Kilimanjaro,inatarajia kuwafikisha mahakamani madereva na makondakta
wanaowatoza abiria nauli kubwa tofauti na zilizopangwa na mamlaka hiyo.
- Polisi nchini Brazil,
wanamshikilia kwa mahojiano rais wa zamani wa nchi hiyo, Luiz da Silva, baada
ya kuipekua nyumba yake na majengo mengine yanayohusishwa naye, ikiwa ni sehemu
ya uchunguzi wa kashfa ya ufisadi inayoikabili kampuni kubwa ya mafuta,
Petrobras.
HABARI KAMILI.
MOSHI
Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro,linamshikilia
mkazi wa kijiji cha Kisangesangeni,wilayani Moshi vijijini,Aboukar Macha,kwa
tuhuma za kumiliki silaha kinyume cha sheria.
Kamanda wa polisi mkoani
Kilimanjaro,Ramadhani Mungi,amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa jana mchana baada
ya kupekuliwa nyumbani kwake na kukutwa na silaha hiyo aina ya Pistol yenye
namba ADP 0160A ikiwa na risasi mbili.
Kamanda Mungi amesema mtuhumiwa huyo pia
alikutwa na mtutu wa bunduki aina ya Shotgun,akiwa amevificha nyumbani kwake,na
amekuwa akivitumia katika matukio ya uhalifu.
Amesema mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa
mahakamani baada ya taratibu kukamilika.
Katika tukio lingine jeshi la polisi
limewakamata wakazi wa Msaranga,wikayani Moshi,Philipo John na Sist Philipo,kwa
tuhuma za kukutwa na pombe haramu aina ya Gongo lita 40.
Kamanda Mungi amesema watuhumiwa hao pia
walikutwa na mitambo mine ya kutengenezea pombe hiyo,ambapo watafikishwa
mahakamani baada ya taratibu kukamilika.
DAR ES SALAAM.
Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi
Usafiri wa Majini na Nchi Kavu,SUMATRA, mkoani Kilimanjaro,inatarajia kuwafikisha
mahakamani madereva na makondakta wanaowatoza abiria nauli kubwa tofauti na
zilizopangwa na mamlaka hiyo.
Kaimu Afisa Mfawidhi wa
mamlaka hiyo,mkoani Kilimnjaro,Bw.Tadei Mwita,amesema hayo kujibu hoja ya mkazi
wa mkoa huo,kuhusu magarina ya daladala zinazosafari kati ya Moshi Mjini na Himo,
kuwatoza nauli ya shillingi 1000 abiria wanaoshuka Kiboriloni, Sango
Pumuani na Kawawa road, tofauti na nauli iliyopangwa na SUMATRA katika vituo
hivyo.
Mwita amesema kuanzia
wiki ijayo wadau wote watakaoomba leseni kwa ajili ya usafirishaji
wa abiria ndani ya mkoa ,watahitajika kuonyesha nauli watakazo toza abiria
katika vituo vya katikati kabla ya kufika kituo cha mwisho cha safari zao.
Amesema hivi sasa
SUMATRA Mkoa wa Kilimanjaro imeanzisha utaratibu wa kuwataka wadau
wote wanaotarajia kuanza kutoa huduma za usafiri wa daladala, kuonyesha nauli
watakazo toza katika vituo vya katikati kabla ya kufika kituo cha mwisho.
MOSHI.
Imeelezwa kuwa
utekelezaji wa ahadi ya rais Dk John Magufuli kulinda viwanda vya ndani,
imekuwa chachu kwa kiwanda cha sukari TPC wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro,
na kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni
kumi ,kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda hicho.
Afisa mtendaji utawala
wa TPC, Jafary Ali ,amesema hayo wakati akizungumzia uzalishaji kiwandani hapo
,wakati wa ziara ya kamati ya ulinzi na usalama mkoani Kilimanjaro
iliyotembelea kiwanda hicho.
Ally amesema wanaamini
kuwa sukari ya TPC haiuzwi katika mikoa ya kanda ya kaskazini pekee ,na kwamba
ipo mifuko maalumu yenye rangi ya njano ambayo inasambwazwa hadi katika mikoa
ya Tabora na Shinyanga, huku wafanyabiashara wa Mtwara nao wakihitaji bidhaa
hiyo.
Akizungumza na
menejimenti ya TPC baada ya kukagua maghala ya kiwanda hicho na yale ya Kahe,
mkuu wa mkoa, Amos Makalla aliwahakikishia kwamba serikali itaendelea kuvilinda
viwanda vya ndani.
Unaendelea kusikiliza taarifa ya habari kutoka kibo
fm,zifuatazo ni habari za kimataifa.
SEOL
Kiongozi
wa Korea Kaskazini ,Kim Jong-un ,amevitaka vikosi vya taifa hilo vijiandae
kutumia silaha za nyuklia wakati wowote,kuanzia sasa.
Kiongozi huyo amewaambia viongozi wa
kijeshi, kwamba North Korea itabadilisha hali yake ya kijeshi, na kuwa tayari
hata kutekeleza mashambulio ya kuzuia hatari, shirika la habari la KCNA
limesema.
Umoja wa Mataifa umewekea taifa hilo
vikwazo vikali zaidi, baada ya Prongyang kufanya majaribio ya nyuklia na
makombora ya masafa marefu.
Shirika l habari nchini humo,KCNA,limeripoti
kuwa Kim alikuwa akizungumza wakati wa zoezi la kijeshi hapo jana,ambapo inaaminika
huo ulikuwa wakati ambao makombora hayo yafyatuliwa.
BRASISLIA.
Polisi nchini Brazil, wanamshikilia kwa
mahojiano rais wa zamani wa nchi hiyo, Luiz da Silva, baada ya kuipekua nyumba
yake na majengo mengine yanayohusishwa naye, ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa
kashfa ya ufisadi inayoikabili kampuni kubwa ya mafuta, Petrobras.
Msemaji wa kiongozi huyo ,Jose
Crispiniano, amethibitisha kuwa polisi wako kwenye majengo yanayomilikiwa na
Silva, ikiwemo nyumba yake na taasisi yake ya misaada wake Silva alizungumza na
polisi akiwa kwenye kituo cha polisi kwenye uwanja wa ndege wa Sao Paulo.
Polisi inasema kuhojiwa kwa rais huyo wa
zamani aliyejizolea umaarufu wa kuwawakilisha makabwela kwenye uongozi wake, ni
sehemu ya uchunguzi wao unaohusisha watu na taasisi nyengine 44 kwenye kashfa
maarufu iliyopewa jina la Car Wash, ambapo zaidi ya dola bilioni mbili za
Kimarekani zililipwa kwa njia ya rushwa kupata kandarasi za Petrobras.
JERUSALEM.
Vikosi vya kijeshi vya Israel,vimevunja
majengo kadhaa ya Wapalestina, ikiwemo shule moja, kaskazini mwa Ukanda wa
Magharibi, na kuziacha familia kumi zikiwa hazina mahala pa kukaa.
Taarifa iliyotolewa leo na Umoja wa
Mataifa inasema uvunjwaji huo ulifanyika kwenye kijiji cha Khirbet Tana, kusini
mwa mji wa Nablus, ambapo majengo 41 yalivunjwa, na kupelekea Wapalestina 36,
miongoni mwao watoto 11, kupoteza makaazi yao.
Hata hivyo, idara ya shughuli za serikali
ya Israel kwenye mamlaka ya Palestina, inasema majengo yaliyovunjwa ni 20,
ikidai kuwa walitoa tangazo muda mrefu kabla ya uvunjwaji wenyewe.
Israel inakalia asilimia 60 ya kile
kinachoitwa Area C, kwenye ardhi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi, ambako
ni shida kwa Wapalestina kupata kibali cha ujenzi.
Kabla ya
kumaliza taarifa hii ya habari sikiliza tena mukhtsari wake.
- Jeshi la polisi mkoani
Kilimanjaro,linamshikilia mkazi wa kijiji cha Kisangesangeni,wilayani Moshi
vijijini,Aboukar Macha,kwa tuhuma za kumiliki silaha kinyume cha sheria.
- Mamlaka ya Udhibiti
na Usimamizi Usafiri wa Majini na Nchi Kavu,SUMATRA, mkoani
Kilimanjaro,inatarajia kuwafikisha mahakamani madereva na makondakta
wanaowatoza abiria nauli kubwa tofauti na zilizopangwa na mamlaka hiyo.
- Polisi nchini Brazil,
wanamshikilia kwa mahojiano rais wa zamani wa nchi hiyo, Luiz da Silva, baada
ya kuipekua nyumba yake na majengo mengine yanayohusishwa naye, ikiwa ni sehemu
ya uchunguzi wa kashfa ya ufisadi inayoikabili kampuni kubwa ya mafuta,
Petrobras.
Mwisho wa
taarifa ya habari kutoka kibo fm,jiunge nasi tena kesho saa nne kamili
kusikiliza kibo fm asubuhi.