Video Information
TAARIFA
YA HABARI JAN,23,2016.
HII NI
TAARIFA YA HABARI KUTOKA KIBO FM.
MIMI
NI……………………………..
KWANZA
MUKHTASARI WAKE.
-
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo kitovu cha nchi na kwamba kila Mtanzania ameelekeza
jicho lake pale kwa sababu anasubiri kupata huduma ya msingi.
- Watu watatu wamefariki dunia,na wengine 35 kujeruhiwa vibaya baàda
ya basi walilokuwa wakisafiria kutokea jijini Dar es salaam kuelekea Morogoro,
mali ya kampuni ya bm yenye namba za usajili T916 BQX kuligonga ubavuni lori la
mizigo lenye namba T184 CGX na kuangukia kwenye bonde pembeni ya barabara na
kupinduka mara nne.
HABARI
KAMILI.
DODOMA.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo kitovu cha nchi na kwamba
kila Mtanzania ameelekeza jicho lake pale kwa sababu anasubiri kupata huduma ya
msingi.
Ametoa kauli hiyo juzi wakati akizungumza na
wakurugenzi, wakuu wa taasisi na watumishi wa Ofisi ya Rais – Tamisemi kwenye
mkutano uliofanyika ofisi ya Tamisemi mjini Dodoma.
Waziri Mkuu ameitaka ofisi hiyo ihakikishe
inaisimamia vizuri mikoa na halmashauri ili Serikali iweze kupata matokeo
mazuri na tarajiwa na kuongeza kuwa jukumu kubwa lililopo hivi sasa katika
Mamlaka za Serikali za Mitaa ni kuhakikisha kuwa zinabuni vyanzo vipya vya
mapato na kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato ya serikali.
Pia amesema Serikali ya Awamu ya Tano imekusudia
kuwahudumia ipasavyo Watanzania wenye uelewa tofauti na matakwa tofauti na kwa
kuanzia Serikali imeanza kuwajenga watumishi wa Serikali kutambua kuwa wao ni
wahudumu wa wananchi hivyo inawapasa kuwahudumia vema.
MOROGORO.
Watu watatu wamefariki dunia,na
wengine 35 kujeruhiwa vibaya baàda ya basi walilokuwa wakisafiria kutokea
jijini Dar es salaam kuelekea Morogoro, mali ya kampuni ya bm yenye namba za
usajili T916 BQX kuligonga ubavuni lori la mizigo lenye namba T184 CGX na
kuangukia kwenye bonde pembeni ya barabara na kupinduka mara nne.
Kamanda wa polisi mkoa wa
morogoro Leonard paul amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa basi
ambalo lilishindwa kupunguza mwendo baada ya lori ambalo lilikua linaovateki
lori lililoaribika huku na majeruhi kulalamikia wizi uliofanywa na waliofika
eneo la tukio baada ya ajali
Daktari bingwa wa upasuaji katika
hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro,Francis Semwene amesema watu wawili
wamefariki katika eneo la ajali na mmoja amefariki akiwa hospital hapo huku
majeruhi wanne kati ya 35 wakiwa kwenye hali mbaya kutokana na kuumia sana
ambapo amesema italazimika kuwakata baadhi ya viungo iwapo watashindikana
kushonwa.
TANGA.
Mpango wa taifa wa kueneza nishati
itokanayo na kinyesi cha wanyama umeelezwa kuwa na manufaa makubwa kwa wakazi
wa maeneo ya vijijini kwani licha ya kuwapatia mbolea bora, bayogesi
inawawezesha kupata nishati ya kupikia, kutoa wanga na hata mabaki yatokanayo na
uzalishaji bayo gesi kutumika kama dawa dhidi ya mbu na wadudu wengine
waharibifu.
Akizungumza katika sherehe ya
uzinduzi wa awamu ya pili ya mpango wa kueneza bayogesi nchini katika kijiji
cha Boza, wilaya ya Pangani mkoani Tanga hivi karibuni, mmoja wa wanakijiji
walio na mtambo wa bayogesi ameelezea anavyonufaika.
Kwa upande wake mratibu wa mpango
huo, Lehada Cyprian Shila, amesema tokea wazindue mpango wa uenezi wa bayogesi
wa taifa mwaka 2009 wamekwifanikiwa kujenga mitambo ya bayogesi ipatayo 20, 700.
Mpango wa taifa wa kueneza matumizi
ya nishati jadidifu ya bayogesi ulianza mwaka2009, ikiwa ni sehemu ya mpango wa
kueneza nishati barani Afrika ulionufaisha mataifa matano yakiwemo Tanzania na
Burkina Faso.
ZANZIBAR.
Shule ya msingi ya Kisiwandui iliyopo
visiwani Zanzibar, inakabiliwa na uhaba wa vifaa mbalimbali vya kufundishia
wanafunzi wasioona na wale wenye ulemavu wa viungo na kuwaomba wafadhili na
wasamaria wema kujitokeza na kuwasaidia wanafunzi hao ili waweze kusoma katika
mazingira mazuri na kujihisi kama wenzao.
Matatizo hayo yamebainika wakati wa
hafla fupi ya makabidhiano ya msaada wa shilingi milioni 20 zilizotolewa na
kampuni ya simu ya mkononi ya Zantel kwa ajili ya kununulia vifaa mbalimbali
vya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya Kisiwandui.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi
mfano wa hundi hiyo ya shilingi milioni 20, Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Bwana
Beneit Janin amesema msaada huo utasaidia kupunguza baadhi ya matatizo
yaliyokuwa yakiikabilia shule hiyo na kutoa ahadi kuwa Kampuni yake itaendelea
kutoa misaada kwa wanafunzi hao ili waweze kusoma katika mazingira mazuri.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi,
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi Taifa Khamis Ahmed amesema licha ya kukabiliwa na
changamoto mbalimbali, wanafunzi hao wamefanikiwa kufanya vyema katika masomo
yao na kuendelea katika masomo ya elimu ya juu.
Akitoa neno la shukrani kwa niaba
ya wanafunzi wenzake, Mwanafunzi Mbarouk Nassor Mbarouk amesema miongoni mwa
matatizo yanayowakabili ni pamoja na ukosefu wa fimbo nyeupe na vifaa vya
kuzuia mavumbi kwa wanafunzi wasioona.
Unaendelea
kusikiliza taarifa hii ya habari kutoka kibo fm,zifuatazo sasa ni habari za
kimataifa.
ADDIS
ABABA.
Mkutano
huo unafanywa siku moja baada ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa kukutana na rais wa
Burundi, Pierre Nkurunziza, ambaye uamuzi wake wa kugombea muhula wa tatu wa
uongozi ulizusha miezi kadha ya ghasia.
Mwakilishi
wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Samantha Power, alisema mazungumzo hayo
hayakufanikiwa kama alivyotaraji.
Rais
Nkurunziza alikataa wito wa mazungumzo, upatanishi na kikosi cha Umoja wa
Afrika kuingilia kati.
PORT-AU-PRINCE.
Tume ya uchaguzi nchini Haiti imearisha marudio ya uchaguzi wa urais kwa
miaka mitatu sasa, licha ya Rais Michel Martly kutangaza kuwa uchaguzi huo
utaendelea.
Tume ya
uchaguzi ilisema kuwa ilifanya uamuzi huo kutokana na ukosefu wa usalama.
Kumekuwa na
hali ya wasiwasi juu ya marudio ya uchaguzi huo wa Urais, kukiwa na maandamano
ambapo makundi ya upinzani yamedai kuwa kuna njama ya kuiba kura.
Rais Martelly
anazuiwa katika kugombea Urais huo.
Utawala wake
unamalizika kikatiba baada ya majuma matatu na kuna hofu kuwa uchaguzi
usipofanywa huenda kukazuka ghasia.
HARARE.
Bwana
Mugabe, mwenye umri wa miaka 91, amesema ni mzima kama kigongo.
Anakutana
na kiongozi mwengine mkongwe wa Afrika, Teodoro Obiang Nguema wa Equatorial
Guinea, ambaye anafanya ziara rasmi nchini Zimbabwe.
Rais
Nguema ameongoza Equatorial Guinea kwa miaka 36, mwaka mmoja zaidi ya Rais
Mugabe.
OTTAWA.
Mshukiwa
mwanamume ametiwa mbaroni nje ya Shule ya Kijamii ya Loche, ambako kisa hicho
kilitokea.
Polisi
pia wanaendelea kufanya uchunguzi katika tulio jingine la ufyatulianaji risasi
katika kijiji cha watu 3,000 nchini humo.
Waziri
Mkuu wa Canada, Justin Trudea, ametaja vifo hivyo kama hofu kubwa inayoweza kumkumba
mzazi yeyote.
Mauaji
ya watu wengi kwa bunduki nchini Canada si jambo la kawaida , ambako sheria za
kuthibiti bunduki ni kali zaidi kuliko Marekani.
Kabla ya kumaliza taarifa hii ya habari
sikiliza tena mukhtasari wake.
-
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo kitovu cha nchi na kwamba kila Mtanzania ameelekeza
jicho lake pale kwa sababu anasubiri kupata huduma ya msingi.
- Watu watatu wamefariki dunia,na wengine 35 kujeruhiwa vibaya baàda
ya basi walilokuwa wakisafiria kutokea jijini Dar es salaam kuelekea Morogoro,
mali ya kampuni ya bm yenye namba za usajili T916 BQX kuligonga ubavuni lori la
mizigo lenye namba T184 CGX na kuangukia kwenye bonde pembeni ya barabara na
kupinduka mara nne.
Mwisho wa taarifa ya habari kutoka kibo
fm,jiunge nasi tena kesho saa nne kamili kusikiliza kibo fm asubuhi.