Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

WANAFUNZI WA DARASA LA AWALI 139 WAKOSA DARASA LA KUSOMEA

Views:
Video Information
kiongosi_88164.jpg
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mijimwema mjini Njombe, mkoani Njombe, Monica Kiongosi wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi baada ya kikao cha kufungia shule, ambapo pamoja na mambo mengine wazazi walipewa ripoti za watoto wao. Shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 818 na walimu 20 amabpo mwalimu wakiume ni mmoja tu. Changamoto nyingine ni upungufu wa madawati, matundu ya vyoo yaliopo ni matundu 12, nyumba za walimu pamoja na madarasa.
wanafunzi_e60a2.jpg
Wanafunzi wa shule ya Msingi Mjimwema mjini Njombe, mkoani Njombe wakiosha sahani kisimani kabla ya kwenda kupiga foleni ya kupata chakula cha mchana ambapo mara nyingi ni kande. Shule hiyo inatumia maji ya kisima baada ya mfumo wa maji ya bomba kuchakaa.
zahanti_817de.jpg
Msimamizi wa Zahanati ya Mjimwema, Debora Kyejo (kushoto) akionyesha baadhi ya dawa zilizopo katika chumba cha dawa wakishirikiana na Melisiana Mhagama walipotembelewa na mwandishi wa gazeti la kwanzajamii hivi karibuni. Zahanati hiyo ilijengwa kwa nguvu za wananchi na ina changamoto mbalimbali kama vile upungufu wa watumishi waliopo ni watumishi wa tatu, haina daktari, haina vitanda vya kufanyia uchunguzi (examination beds) na vitanda vya kujifungulia vilivyopo ni vitanda viwili na  umeme.
darasa_4721e.jpg
Mafundi wakiendelea kuezeka mabati kwenye darasa la awali ambalo limeanza ujenzi wake kwa muda mrefu bila kukamilika. Shule ya Msingi Mjimwema haina darasa la awali inatumia chumba kimoja kwa ajili ya wanafunzi 139 ambapo hata hivyo wanalazimika kusoma kwa zamu. Wanafunzi hao wanakalia madawati ya kawaida badala ya mawadati kwa jili yao maalum.
foleni_6fe58.jpg
Wanafunzi wakiwa katika foleni ya kupata chakula cha mchana.
kande_875d0.jpg
Mpishi akiendelea kupita chakula cha wanafunzi ambapo mara nyingi ni kande.
Similar Videos