Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

KIUNGO WA ZAMANI LIVERPOOL: DANNY MURPHY ASTAAFU!

Views:
Video Information

DANNY_MURPHYKIUNGO wa zamani wa Liverpool, Danny Murphy, amethibitisha kustaafu baada ya kucheza Soka kwa Miaka 20.
Murphy hajacheza tangu Msimu uliopita na sasa ameamua kutangaza rasmi kuwa amestaafu kucheza Soka baada ya kuacha kucheza tangu Mwezi uliopita.
Murphy, mwenye Miaka 36, aliichezea Liverpool Mechi 249 kati ya Mwaka 1997 na 2004 na kwenye Msimu wa 2000/01 yeye ndie alikuwa nguzo kubwa walipotwaa Kombe la Ligi, FA CUP na UEFA CUP kwa mpigo.
Mbali ya kuichezea Timu ya Taifa ya England mara 9, pia amezichezea Klabu za Crewe Alexandra, Charlton Athletic, Tottenham Hotspur, Fulham na Blackburn Rovers.
Akitoboa habari hizi za kustaafu kwake, Murphy amesema kupitia Tovuti ya Klabu ya Liverpool: “Huyu ni mimi, Miaka 20, nimemaliza. Nilikuwa na maisha mazuri ya Soka na nitayafurahia.”
Murphy na Klabu yake ya mwisho, Blackburn Rovers, kabla Msimu huu mpya kuanza, walifikia makubaliano ya kuvunja Mkataba kati yao.
Murphy amesema: “Kumekuwa na taarifa kwenye Vyombo vya Habari zikiuliza kama bado nacheza au nipo lakini niliamua muda nyuma kuwa sasa nastaafu lakini sikutangaza rasmi. Sasa  natangaza rasmi!”
Similar Videos