Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

LIGI KUU VODACOM: LEO YANGA MBEYA, SIMBA DAR!

Views:
Video Information
VPL_2013-14_LOGO-NEWBAADA ya Wiki mbili za ‘Vakesheni’ kuipisha Taifa Stars kucheza Mechi ya Kundi lake la kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwakani dhidi ya Gambia, Timu zote 14 za Ligi Kuu Vodacom zitakuwa Viwanjani hii leo kucheza Mechi zao za tatu za Ligi.
Mabingwa Watetezi, Yanga, wako huko Mbeya kucheza kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine dhidi ya Mbeya City, Timu iliyopanda Daraja Msimu huu.
Katika Mechi mbili za Ligi walizocheza, Yanga walianza kwa kuifunga Ashanti United 5-1 na kutoka Sare 1-1 na Coastal Union wakati Mbeya City walitoka Sare 0-0 na Kagera Sugar na kuifunga Ruvu Shootinga Bao 2-1.
Vigogo wa Soka Nchini, Simba, wao watacheza Jijini Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kwenye Ligi Msimu huu kwa kucheza Uwanja wa Taifa na Timu kali ya Mtibwa Sugar, ambayo imeanza kwa ushindi na Sare kama Simba ambayo ilitoka 2-2 na Rhino Rangers na kisha kuitungua JKT Oljoro Bao 1-0.
Viingilio kwa Mechi hii ya Simba na Mtibwa Sugar ni Shilingi 5,000 Viti vya Bluu na Kijani, Sh. 8,000 Viti vya Rangi ya Chungwa, Sh. 15,000 VIP C na B wakati VIP A itakuwa Sh. 20,000.
Nao Azam Fc, ambao Msimu uliopita walimaliza Nafasi ya Pili nyuma ya Mabingwa Yanga na kuiacha Simba ikamate Nafasi ya Tatu, ipo Ugenini huko Kaitaba Stadium kucheza na Kagera Sugar.
Vinara wa Ligi, JKT Ruvu, Timu pekee iliyoshinda Mechi zake zote mbili za Ligi, watakuwa kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam Uwanja wa Azam Complex kucheza na Ashanti United ambayo imepanda Daraja Msimu huu lakini hadi sasa hali yao ni taabani baada ya kuchapwa Mechi zote mbili mfululizo.
VPL-MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
JKT Ruvu
2
2
0
0
5
6
2
Yanga SC
2
1
1
0
4
4
3
Azam FC
2
1
1
0
2
4
4
Coastal Union
2
1
1
0
2
4
5
Mtibwa Sugar
2
1
1
0
1
4
6
Simba SC
2
1
1
0
1
4
7
Mbeya City
2
1
1
0
1
4
8
Ruvu Shooting
2
1
0
1
2
3
9
Mgambo Shooting
2
1
0
1
-1
3
10
Kagera Sugar
2
0
1
1
-1
1
11
Rhino Rangers
2
0
1
1
-2
1
12
JKT Oljoro
2
0
0
2
-3
0
13
Ashanti UTD
2
0
0
2
-5
0
14
Prisons FC
2
0
0
2
-6
0
**MSIMAMO TOKA TFF

VPL: LIGI KUU VODACOM
MATOKEO:
Jumamosi Agosti 24
Yanga 5 Ashanti 1
Mtibwa Sugar 1 Azam FC 1
JKT Oljoro 0 Coastal Union 2
Mgambo JKT 0 JKT Ruvu 2
Mbeya City 0 Kagera Sugar 0
Ruvu Shooting 3 Prisons 0
Rhino Rangers 2 Simba 2

Jumatano Agosti 28
Mtibwa Sugar 1 Kagera Sugar 0
Rhino Rangers 0 Azam FC 2
Mbeya City 2 Ruvu Shootings 1
Mgambo JKT 1 Ashanti United 0
JKT Oljoro 0 Simba 1
Yanga 1 Coastal Union 1
JKT Ruvu 3 Prisons 0
Similar Videos