Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

WARIOBA ASIBEZWE

Views:
Video Information
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji mstaafu, Joseph Warioba, inawatakia mema Watanzania hivyo iungwe mkono.
Chama hicho kimesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), hakitaki mabadiliko hapa nchini ndiyo maana kinabeza na kimejipanga kukwamisha baadhi ya mapendekezo yaliyomo kwenye rasimu ya Katiba mpya.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, katika mikutano ya mabaraza ya wazi ya Katiba mpya.
Alisema viongozi na makada wa CCM wamekuwa wakiibeza rasimu hiyo iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Joseph Warioba kwa kuihofia kuwa inakiondoa madarakani chama chao.
Similar Videos