Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

katika page ya chadema facebook

Views:
Video Information
Bila shaka hali hii ndiyo inayowatisha CCM na kuwakatisha tamaa kabisa. Wananchi kwa vitendo wameendelea kuiasi na kuikataa CCM na vitisho vyake vyote, ikiwemo vya kuwatumia baadhi ya mabosi wa Jeshi la Polisi, kufanya hujuma dhidi ya Vuguvugu la Mabadiliko, ambapo hivi karibuni imeshuhudiwa ikifikia hali mbaya zaidi pale 'wahujumu' walipoamua kutumia mabomu ya machozi, mabomu ya kivita na bunduki za kivita zenye risasi za moto!
Wananchi wameendelea kusimama na upande unaowatetea, kuwasemea na kuwawakilisha. Wamesimama upande wa watetezi wa haki, wapinga dhuluma.
Moja ya malengo ya hujuma za hivi karibuni ilikuwa ni kuwatisha wananchi waogope kuhudhuria mikutano ya CHADEMA. Imeshindikana. Watanzania wameshaamua kusonga mbele. Hakuna kitakachowarudisha nyuma katika kuisaka haki, kutafuta mabadiliko ya utawala na mfumo.
Mkutano wa kwanza wa CHADEMA mara baada ya shambulio la kigaidi la bomu pale Soweto, Arusha, ulifanyika Songea, ikafuatiwa na Shinyanga, kisha Tabora, ikiwa ni shughuli za ukamilishaji wa kuzindua Kanda ya Kusini (Ruvuma, Mtwara na Lindi) Kanda ya Ziwa Mashariki (Simiyu, Shinyanga na Mara) na Kanda ya Magharibi (Kigoma, Tabora na Katavi).
Kote huko wananchi, Watanzania wote, bila kujali tofauti zao, za kisiasa, kiuchumi na kijamii, wameendelea kuunganishwa na matatizo yao ya msingi kama jamii moja, iliyokwamishwa na kunyimwa fursa ya kuendelea, kutokana na uongozi mbovu wa CCM, uliokumbatia ufisadi, ubadhirifu, dhuluma kwa wananchi walioiamini hapo kabla na sasa umeanza kuwagawanya kwa sera zinazopalilia ubaguzi wa dini, ukanda na ukabila.
Ushahidi wa picha, ambazo zinaonesha wananchi wa maeneo mbalimbali, maelfu kwa maelfu wakisikiliza hoja na kushiriki kwenye Mabaraza ya Wazi ya CHADEMA, kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya, unapaswa kuwa somo kubwa kwa CCM na vibaraka wao wachache kwenye vyombo vya dola, ambao wameamua kutumika na kutia doa majeshi yetu na askari wetu wengine (wengi) waaminifu na watiifu kwa wananchi wanaopaswa kuwatumikia kwa kutenda na kulinda haki kwa kufuata katiba, sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Picha; wananchi walivyoipokea CHADEMA, utoaji wa maoni yao Rasimu ya Katiba Mpya;
Hapa ni mikutano ya jana kuanzia Njombe, Makambako, Ilula na Iringa mjini...
Similar Videos