Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

HATIMAYE : Bale avunja rekodi ya uhamisho wa dunia

Views:
Video Information

 

MADRID, HISPANIA
NDANI ya saa 24 zijazo kitabu kipya cha historia katika soka kitafunguliwa wakati Gareth Bale atakapotangazwa kuwa mchezaji ghali zaidi duniani katika uhamisho wa Pauni 94 milioni kutoka Tottenham kwenda Real Madrid.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Spurs, Franco Baldini, ametua jijini  Madrid tangu juzi Alhamisi kwa ajili ya kukamilisha uhamisho huo ambao utavunja rekodi iliyowekwa na winga wa Ureno, Cristiano Ronaldo aliyehamishwa kwa Pauni 80 milioni kutoka Manchester kwenda Madrid mwaka 2009.
Awali, ofa ya Pauni 85 milioni ya Real Madrid ilikataliwa mwezi uliopita, kabla ya ofa ya ongezeko la mchezaji mmoja ambaye ni Fabio Coentrao nalo kukataliwa. Lakini sasa mambo yamenyooka.
Spurs inatazamiwa kupokea kiasi cha Pauni 59 milioni mbele kama malipo ya awali kabla ya kupokea tena kiasi cha Pauni 12 milioni kitakachokwenda kwa mafungu manne kukamilisha dau zima itakapofika mwaka 2017.
Nyota huyo anatazamiwa kutambulishwa rasmi katika Uwanja wa Santiago Bernabeu mapema wiki ijayo mbele ya maelfu ya mashabiki wa timu hiyo ambao wamezoea utamaduni huo kwa miaka nenda rudi.
Tayari maduka ya Real Madrid yameanza kuuza jezi ya Bale namba 11 na hata kabla mchezaji huyo hajatambulishwa rasmi, picha ya jezi yake hiyo ilionekana katika tovuti rasmi ya Real Madrid tangu Alhamisi usiku.
Kuuzwa kwa Bale kunaweka uwiano mzuri wa hesabu za Tottenham ambayo mpaka sasa imetumia Pauni 60 milioni kuwanasa mastaa mbalimbali kwa ajili ya kusaka nafasi ya Top Four.
Tayari imevunja rekodi yake ya uhamisho kwa kumnasa mshambuliaji wa Valencia, Roberto Soldado, kwa kiasi cha Pauni 26 milioni huku pia ikiwanasa, Nacer Chadli na Paulinho.
Pia kipo mbioni kumnasa mshambuliaji wa AS Roma, Erik Lamela na kiungo wa Anzhi Makachkala, Willian.
Kwa Madrid, hilo litakuwa jibu lao kubwa kwa Barcelona ambayo katika kipindi hiki cha uhamisho wa wachezaji ilifanikiwa kuipiga bao Madrid kwa kufanikiwa kuinasa saini ya staa wa Santos, Neymar kwa kiasi cha Pauni 50 milioni.
Huu ni mwendelezo wa mpango maalumu wa Rais wa Madrid, Fiorentino Perez, ambaye chini yake mashabiki wa Santiago Bernabeu wameshuhudia wachezaji wenye majina makubwa kama Zinedine Zidane, Ronaldo de Lima, David Beckham, Luis Figo na Cristiano Ronaldo wakitua kuichezea timu hiyo.
Similar Videos