Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

HII NI KAMA MAKALA

Views:
Video Information


Watu wengi sana tumezoea kuona migogoro ya ardi ikiwa ni makabila kwa makabila lakini imeonekana kutokea kwa migogoro kati ya ndugu kwa ndugu .
Ilikuwa ni jumamosi ya tarehe 09-02-2013 kulikuwa na mkutano mkubwa ambao ulikutanisha baadhi ya viongozi wa kijiji pamoja na viongozi wa ukoo.mwenyekiti wa ukoo alikuwa ni Philip Tesha na mwenyekiti wa kijiji alikuwa ndugu Eleutery Swaty kuhakikisha ndugu hao wamepatana.
              JINSI ILIVYO KUWA MWANZO HADI MWISHO
Upatikanaji wa shamba Laurenti Tesha aliweza kumpatia Michaeli tesha shamba kama ndugu yake lakini alitokea ndugu mwingine ambaye ni Faustine Tesha akamwambia eneo ambalo umepewa sio sahihi kwa wewe kuishi kwani lilikuwa ni eneo la bondeni na kumpatia nkipande cha eneo.
Kwa upande wa mlalamikaji ambaye ni familia ya Faustine Tesha wamesema eneo hilo alipewa kwa muda hadi atakapo pata eneo rasmi la kuishi lakini hakuna maandishi ambayo yanaonyesha makabidhiano.tangu mwaka 1979 ndiyomwaka ambao waliweza kupeana eneo hilo la shamba  na pia hakuna maandishi yanayothibitisha hilo.
Pia inaonekana chanzo cha mogogoro hiyo inasemekana ni mlalamikiwa Michael Tesha kutengeneza msingi wa nyumba na walalamikaji kusema kuwa amesogeza mpaka wa shamba lao na kutaka kumfukuza katika eneo alilopewa na marehemu ndugu yake Faustine Tesha.
Wakati kikao kinaendelea ilifika mahali kukatawaliwa na hasira kwa upande wa walalamikaji ndipo mwenyekiti wa kijiji cha Njari Eleutery Swaty akawanyamazisha na kurudisha hali ya utulivu pamoja na amani na kuweza kuendelea na kikao.
Ilionekana wazi kuwa familia ya Faustine Tesha  kwenda kupanda migomba pamoja na kahawa katika eneo alilopewa Michael Tesha na ni karibu na nymba yake anayoishi kwa sasa ambayo mtoto wa Michael anataka kujenga nyumba.
Chanzo kingine ambacho kimeonekana ni ndugu Michael hajawahi kutoa hata kitu kwa familia ya Faustine na kuonyesha kama shukrani kwa kupewa eneo la kuishi pia marehemu faustine alipofariki hakuna aliye kwenda kutoa neno lolote kama kuna sehemu kapewa na marehemu na amefariki itakuaje.
Kikao kilifanyika mbali na eneo la tukio na kulazimu aliye kuwepo pale kwenye kikao kwenda kuangalia eneo wanalo gombania .Vilevile kulikuwa na barua batili ya kuonyesha kikao cha ukoo wa Tesha pamoja na mwenyekiti feki aliye kuwa amesaini barua hiyo amabaye ni William Tesha na barua hiyo dhahiri shahiri ilonekana kuegemea upande mmoja.
Pia eneo wanalogombania awamu Michael alikuwa ametengeneza nyumba ya ng”ombe na ndipo alibomoa kwa ajili ya kujenga nyumba ya mwanaye.Na mwenyekiti wa kijiji aliweza kusema kuwa kama hawataki aishi eneo hilo waweze kumfidia lakini hakuna aliye afiki kitendo hicho.
Baada ya ukweli kuonekana familia ya Faustine waliweza kusema kuwa wamemwachia eneo hilo na pi mwenyezi mungu aangalie kama ni haki huku ikiwa ni kwa shingo upande siyo kwa nia nzuri wala moyo mmoja.
MWISHO kikao kilimalizika kwa uongozi wa kijiji kumwambia Michaeli aweze kuita baraza la ardhi kwaajili ya kuweka mipaka sahihi ili kuepusha usumbufu na kuishi katika eneo lake bila matatizo yoyote na endapo kuna tatizo litakalo jitikeza aweze kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji.
                                                                           DEOGRATIUS KESSY
Similar Videos