Video Information
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Togo
Algeria hata hivyo huenda ikakosa huduma za nyota wake Sofiane Feghouli, ambaye alijeruhiwa wakati wa mechi ya siku ya Jumanne dhidi ya Tunisia.
Wachezaji wa Algeria
Togo, kwa upande wake, haina matatizo yoyote ya majeraha na huenda kikosi kilichocheza mechi yao ya kwanza ndicho kitakachocheza hii leo.
Kundi D imetajwa kundi la mauti
Magwiji hao kutoka Magharibi mwa Afrika nao wanahitaji ushindi katika mechi ya leo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kupiga hatua, katika mashindano hayo.
Mchezaji wa Togo Emmanuel Adebayor
Kocha wa Algeria Vahid Halilhodzic amesema, wamejifunza mengi kutokana na mechi yao ya kwanza na kwa sasa vijana wake na ari ya kushinda ila amekiri kuwa mechi ya leo sawa na mechi ya ufunguzi itakuwa ngumu.
Mkufunzi wa Togo Didier Six naye amesema walifanya mkutano wa dharura baada ya mechi yao ya kwanza ili kujadili yale yaliyokwenda mrama na kupanga mikakati ya kujiimarisha katika mechi zilizosalia za makundi.
bbc swahili