Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

UN: Zimbabwe inahitaji msaada wa mamilioni ya dola

Views:
Video Information

Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa dola milioni 131 zinahitajika ili kukidhi mahitaji ya chakula, maji na mahitajio mengine ya dharura huko Zimbabwe katika mwaka huu wa 2013. Alain Noudehou, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu na Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Zimbabwe ameyasema hayo huko Harare mji mkuu wa nchi hiyo hapo jana. Noudehou amesema hali ya kibinadamu imeimarika kwa kiwango fulani huko Zimbabwe ikilinganishwa na mwaka uliopita, suala ambalo limepelekea kupungua kwa msaada ulioombwa mwaka jana  kwa ajili ya nchi hiyo  na kuwa chini ya dola milioni 197. Uzalishaji wa chakula ulipungua kwa kiasi kikubwa huko Zimbabwe tangu mwaka 2011 kutokana na kuyumba kwa hali ya kiuchumi na kisiasa. Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu na Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Zimbabwe amesema dola milioni 110 kati ya msaada wote wa dola milioni 131 ulioombwa zitatumika kwa ajili ya kuwahudumia watu milioni 1.6 wanaokabiliwa na upungufu wa chakula huko Zimbabwe.
Similar Videos