Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

UJIO MPYA WA CLIMAX BIBO KUTOKA BML

Views:
Video Information
YeS..ni Climax Bibo, Star kutoka  'kruu' ya Mexicana Lacavela, ambaye amedondosha 'single' mpya  akiwa ndani ya Record Lebo  mpya  ya BML chini ya mkali  kitambo kwenye  'game' Benjamin Busungu a.k.a Benjamin wa Mambo Jambo. Akipiga  stori na  teentz.com,  juzi kati, Climax  alifunguka  kuwa  ngoma  hiyo mpya  inakwenda kwa jina la 'Getho Boy' tayari  imeshafanyiwa mpango wa Video na soon itakuwa kwa hewa  mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kuifanyia  Editing.
"Nashukuru  Mungu huu ni ujio wangu mpya  nikiwa kwenye mikono ya BML, binafsi  namkubali sana  Benja na ninajua  tutapiga bao kwa  kile  tunachokifanya  sasa, kikubwa  naomba  fans kuipokea ngoma  hiyo na kuyapitia mashairi ili kuyaelewa zaidi  kupitia  clip yake  hapo  chini" alisema  Climax
Kwa upande wake  C.e.o wa  BML Production,  Benjamini wa Mambo Jambo,  amedokeza kuwa ngoma  hiyo ya Climax 'Getho Boy' pia  itatumika  kama  Soundtrack kwenye movie  ya Coast to Coast iliyoigizwa na mkali Slim Omary aliyecheza na mastaa wengine kibao kama Yussuph Mlela, Hemed Suleiman 'PHD' na mwandada Angel ambayo nayo pia  Soon  itakuwa  mtaani.
Similar Videos