Video Information
MAKALA YA MICHEZO NA
BURUDANI MARCH 05,2016.
HABARI ZA MICHEZO KITAIFA.
Kinara
wa mabao katika Ligi Kuu Bara, Hamis Kiiza wa Simba amesema kesho Jumapili
ataichezea timu yake dhidi ya Mbeya City kwa nguvu kubwa ili afunge mabao mengi
ili asifikiwe na mpinzani wake Amissi Tambwe wa Yanga.
Kiiza
raia wa Uganda hadi sasa amefunga mabao 16 katika ligi kuu akifuatiwa na Tambwe
raia wa Burundi aliyefunga mabao 15. Tambwe leo ataichezea Yanga dhidi ya Azam
FC katika ligi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika
mchezo wa kwanza kati ya timu hizo, Simba ilishinda bao 1-0 kwenye Uwanja wa
Sokoine jijini Mbeya.
Kiiza
alisema: “Najua Mbeya City watanikamia kupita kiasi, mimi nitapambana vya
kutosha kuhakikisha naongeza idadi ya mabao.”
“Kitu
kikubwa ninachotaka kukifanya ili mpinzani wangu Tambwe asinipite ni kutodharau
mechi nitakayoicheza na badala yake ni kutumia kila nafasi nitakayoipata kwenye
kila mechi ya ligi kuu.
“Siyo
kitu rahisi, lakini nitahakikisha ninapambana na kufunga mabao kwenye kila mechi,
nitaanza na mchezo wetu wa Jumapili (kesho) dhidi ya Mbeya City.”
Mbeya
City yenyewe katika ufungaji itawategemea zaidi Raphael Alpha mwenye mabao
matano na Haruna Moshi ‘Boban’ aliyefunga mabao matatu hadi sasa katika ligi.
……………………………………………………………….
Kocha
wa JKT Ruvu, Abdallah Kibadeni amemwambia mwenzake wa Mwadui FC, Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’ aache kuchonga badala yake wakutane uwanjani leo katika mchezo
wao wa Ligi Kuu Bara.
JKT
Ruvu inacheza na Mwadui kwenye Uwanja wa Mabatini, Pwani baada ya kuhama kutoka
Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Kibadeni:
“Ukiwa mwoga maneno ya Julio yanaweza kukupa wasiwasi lakini mimi namwambia
tukutane uwanjani.”
Julio
amekuwa akikisifia kikosi chake namna kilivyo fiti na kinaweza kufanya mambo
kwa uhakika huku akisisitiza hawana hofu na JKT inayosuasua.
Kibadeni
amewahi kuwa kocha wa Julio wakiwa Simba, mara ya mwisho alikuwa bosi wake kwa
kuwa Kibadeni alikuwa kocha mkuu na Julio msaidizi, wote wakatupiwa virago
Simba.
…………………………………………………………………………
Uongozi
wa Coastal Union ya Tanga umesema mara tu wachezaji wao watakaporejea kutoka
Morogoro walipokwenda kucheza na Mtibwa Sugar, watawamalizia madai yao yote ya
fedha zilizobaki.
Wiki
iliyopita wachezaji wa timu hiyo waliandamana kudai walipwe mishahara yao ya
miezi mitatu, ambapo uongozi wao ulijitahidi ukawalipa mshahara mwezi mmoja.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili ya Coastal Union, Salim Bawazir, amesema: “Tutawalipa
wachezaji wetu haki zao zilizobaki wakirejea kutoka Morogoro.”
Wachezaji
Coastal Union waliandamana kutaka kulipwa mishahara yao ya miezi mitatu.
Baadaye
uongozi ulilazimika kuwalipa mshahara wa mwezi mmoja na wenyewe wakaingia
uwanjani na kuichanja Mtibwa Sugar kwa bao 1-0 katika mechi ya kwanza ya Kombe
la Shirikisho.
………………………………………………………………………………..
Vijana
wawili wa Yanga wanaendelea kuja kwa kasi, Simon Msuva na Salum Telela, wameipa
matumaini Yanga kufanya vizuri katika mchezo wao wa leo dhidi ya Azam FC.
Lakini
matumaini yameongezeka baada ya mshambulijiaji mkongwe, Amissi Tambwe naye
kuanza mazoezini pia.
Juzi
Msuva na Telela hawakufanya mazoezi wakiwa majeruhi huku Tambwe akisumbuliwa na
mafua lakini jana asubuhi wote walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gombani.
Pia
Ngoma yeye alirejea Yanga mapema wiki hii akitokea kwao Zimbabwe alipokwenda
katika msiba wa mdogo wake aliyefariki wikiendi iliyopita baada ya kugongana
uwanjani.
Kocha
wa Yanga, Hans van Der Pluijm, alisema wachezaji hao wamerejesha matumaini ya
timu yao kufanya vizuri katika mchezo wa leo dhidi ya Azam na ule unaofuata
dhidi ya African Sports.
“Nilikuwa
kwenye wakati mgumu lakini sasa nimerudi katika matumaini baada ya wachezaji
hawa kurejea katika hali zao za kawaida, nina kikosi imara sasa,” alisema
Pluijm, raia wa Uholanzi.
Hata
hivyo, Pluijm aliwaomba mashabiki wa Yanga kuendelea kuisapoti timu yao ili
iendelee kufanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na michuano mingine. Yanga
imerejea jana jijini Dar es Salaam kutoka Pemba tayari kwa mchezo na Azam.
…………………………………………………………………………………….
Umeona
tabia ya kibabe ya mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma? Basi usifikiri kaanza
juzi au jana, Kocha Mkuu wa Mbeya City, Kinnah Phiri anamjua vizuri
Ngoma,
raia wa Zimbabwe, amekuwa gumzo kwa uwezo wa kufunga mabao na matumizi ya nguvu
awapo uwanjani kiasi cha kuwachosha mabeki wengi wa timu pinzani.
Phiri,
raia wa Malawi, aliliambia Championi Jumamosi kwamba, anamfahamu vizuri Ngoma
tangu alipokuwa anacheza FC Platinum ya Zimbabwe kuwa ni ‘mtu wa kazi’ awapo
uwanjani.
“Namjua
vizuri Ngoma kwamba ni mtu asiye na mzaha anapokuwa mbele ya lango la timu
pinzani, nilimfuatilia wakati naifundisha Malawi kwani ilikuwa kazi yangu
kumjua mchezaji wa nchi jirani.
“Bahati
nzuri sijawahi kukutana naye nikiwa kocha na yeye timu pinzani, ni mtu anayejua
wajibu wake na kama ukimpanga na beki mwenye wasiwasi atafanya anavyotaka,”
alisema Phiri.
……………………………………………………………….
Kocha
Mkuu wa Simba, Jackson Mayanja ana aimani kubwa kikosi chake kitaingusha Mbeya
City, kesho Jumapili lakini nahodha wake, Mussa Mgosi ameenda mbali kwa kusema
uwepo wa Haruna Moshi ‘Boban’ na Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kwenye kikosi cha
wapinzani wao si sababu ya kukosa ushindi.
Mayanja
asema, yeye pamoja na wachezaji wenzake watapambana kuhakikisha
wanashinda mechi ya kesho huku wakiombea leo, Azam FC na Yanga zitoke sare ili
warudi kileleni.
Simba
ipo nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 45 huku
Yanga ikiwa kileleni na pointi 46 sawa na Azam iliyo nafasi ya pili.
“Tupo
vizuri kushinda mechi na Mbeya City tutaomba Yanga na Azam watoke sare kwani
ikiwa hivyo sisi tutarejea kileleni, kikosi kipo vizuri kwa mapambano,” alisema
Mayanja.
Kwa
upande wake, Mgosi alisema watahakikisha wanashinda mechi hiyo bila kujali
uwepo wa Boban na Redondo katika kikosi cha Mbeya City.
“Tunawaheshimu
Boban na Redondo, hawa ni wachezaji wakongwe na wazoefu lakini hawawezi
kutuzuia tusishinde mchezo huu tutapambana kuhakikisha tunashinda,” alisema
Mgosi aliyewahi kucheza nao Simba.
………………………………………………………..
Robo
Fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup)
inatarajiwa kuchezwa wikiendi ya mwisho wa mwezi Machi mwaka huu, huku timu
nane zikichuana kusaka nafasi ya kuingia hatua ya nusu fainali ya michuano
hiyo.
Machi
26, 2016 utachezwa mchezo mmoja ambapo Wachimba dhahabu wa Geita Gold watakua
wenyeji wa wachimba Almasi wa mkoa wa Shinyanga timu ya Mwadui FC katika uwanja
wa CCM Kirumba.
Alhamisi
ya Machi 31, 2016, Young Africans watawakaribisha Ndanda FC katika uwanja wa
Taifa jijini Dar es salaam, huku timu ya Azam FC wakiwa wenyeji wa maafande wa
jeshi la magereza Tanzania Prisons katika uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Mchezo
wa mwisho wa robo fainali utachezwa Aprili 6, 2016 kwa Simba SC kucheza dhidi
ya Coastal Union katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Aprili
7, 2016 itachezeshwa droo ya hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho
(ASFC) mojamoja (live) katika Luninga.
Bingwa
wa michuano ya Kombe la Shirikisho msimu huu, ataiwakilisha Tanzania katika
michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF CC) 2017.
………………………………………………………………………………
MECHI ZILIZOPITA ZA AZAM NA YANGA:
Oktoba 17, 2015
Yanga SC 1-1 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Agosti 22, 2015
Yanga 0-0 Azam FC (Yanga ilishinda kwa penalti 8-7 Ngao ya Jamii)
Julai 29, 2015
Azam 0-0 Yanga SC (Azam ilishinda kwa penalti 5-3 Robo Fainali Kombe la Kagame)
Mei 6, 2015
Azam 2-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Desemba 28, 2014
Yanga SC 2-2 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 14, 2014
Yanga SC 3-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Machi 19, 2014;
Yanga SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 22, 2013;
Azam FC 3-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Februari 23, 2013;
Yanga SC 1-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Novemba 4, 2012;
Azam FC 0-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 10, 2012;
Yanga SC 1-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
January 07, 2012
Azam FC 3-0 Yanga SC (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi)
Septemba 18, 2011;
Azam 1-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 30, 2011;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 24, 2010;
Azam FC 0-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 7, 2010;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 17, 2009;
Azam FC 1-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Aprili 8, 2009;
Yanga SC 2-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 15, 2008;
Azam FC 1-3 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
(Rekodi hii inahusisha mechi za mashindano tu, tangu Azam na Yanga wanaanza kukutana)
Oktoba 17, 2015
Yanga SC 1-1 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Agosti 22, 2015
Yanga 0-0 Azam FC (Yanga ilishinda kwa penalti 8-7 Ngao ya Jamii)
Julai 29, 2015
Azam 0-0 Yanga SC (Azam ilishinda kwa penalti 5-3 Robo Fainali Kombe la Kagame)
Mei 6, 2015
Azam 2-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Desemba 28, 2014
Yanga SC 2-2 Azam (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 14, 2014
Yanga SC 3-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Machi 19, 2014;
Yanga SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Septemba 22, 2013;
Azam FC 3-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Februari 23, 2013;
Yanga SC 1-0 Azam FC (Ngao ya Jamii)
Novemba 4, 2012;
Azam FC 0-2 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 10, 2012;
Yanga SC 1-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
January 07, 2012
Azam FC 3-0 Yanga SC (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi)
Septemba 18, 2011;
Azam 1-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 30, 2011;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 24, 2010;
Azam FC 0-0 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Machi 7, 2010;
Yanga SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 17, 2009;
Azam FC 1-1 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Aprili 8, 2009;
Yanga SC 2-3 Azam FC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
Oktoba 15, 2008;
Azam FC 1-3 Yanga SC (Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara)
(Rekodi hii inahusisha mechi za mashindano tu, tangu Azam na Yanga wanaanza kukutana)
MWELEKEO wa wapi taji la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara litaelekea msimu huu tutaanza kuuona leo baada ya mchezo baina ya timu mbili zinazoongoza mbio za taji hilo.
Yanga, mabingwa watetezi wanatarajiwa kumenyana na Azam FC kuanzia Saa 10:00 jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo ambao mshindi atapanda kileleni na kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi tatu. Zote zina pointi 46, kila moja baada ya kucheza mechi 19, ingawa Yanga wapo kileleni kwa wastani wa mabao.
Ni pambano la pili kuzikutanisha timu hizo mwaka huu, na la tano kwa ujumla msimu huu tangu zilipokutana katika Kombe la Kagame Julai mwaka jana, kila timu ikishinda mara moja na nyingine zote kutoka sare.
Julai 29, mwaka jana, timu ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake iliifunga Yanga SC kwa penalti 5-3 katika Robo Fainali ya Kombe la Kagame kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90.
Agosti 22, mwaka huu, Yanga SC ikalipa kisasi baada ya kushinda kwa penalti 8-7 kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 katika mchezo wa Ngao ya Jamii kabla ya sare mbili mfululizo za 1-1, kwanza kwenye Ligi Kuu Oktoba 17, mwaka jana na baadaye kwenye Kombe la Mapinduzi Januari 5, mwaka huu.
Oktoba 17, mwaka jana Yanga ndio walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 45 kupitia kwa Mzimbabwe Donald Dombo Ngoma aliyepokea krosi ya Juma Abdul na kuwachambua mabeki wa Azam kisha kupachika mpira nyavuni – kabla ya Muivory Coast Kipre Tchetche aliyetokea benchi kipindi cha pili kwenda kuchukua nafasi ya Mkenya Allan Wanga kuifungia Azam bao la kusawazisha dakika ya 83 akimalizia pasi ya Farid Mussa.
Katika mchezo huo, Yanga walipata penati baada ya kipa wa Azam Aishi Manula kumuangusha winga wa Yanga Simon Msuva kwenye eneo la hatari, lakini kiungo Mzimbabwe Thabani Kamusoko akampelekea mikononi kipa wa Azam shuti lake.
Na Januari 5, licha ya Azam FC kucheza pungufu baada ya Azam FC kumpoteza Nahodha wake, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano na refa Mfaume Ali Nassor dakika ya 62, lakini ikamudu kumaliza mechi kwa sare ya 1-1.
Azam FC walitangulia kupata bao dakika ya 58 baada ya shambulizi la kushitukiza – sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo, Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast aliyewakokota mabeki watatu wa Yanga SC hadi karibu kabisa na boksi na kufumua shuti lililompita kipa Deo Munishi ‘Dida’.
Lakini beki Mtogo, Vincent Bossou aliisawazishia Yanga SC dakika ya 83 akimalizia mpira ulioparazwa kwa kichwa na Malimi Busungu baada ya kona ya Simon Msuva.
Na kwa ujumla mchezo wa leo ni 19 wa mashindano kuzikutanisha timu hizo, ikiwemo Ligi Kuu, Kombe la Kagame na Kombe la Mapinduzi, kila timu ikishinda mechi saba, moja kati ya hizo kila timu imeshinda kwa penalti, zimetoka sare mara tano na Yanga imefunga mabao 24, wakati Azam imefunga mabao 23.
Makocha wa timu zote, Stewart John Hall raia wa Uingereza anayefundisha Azam FC na Mholanzi Hans vad der Pluijm wa Yanga wanajua mchezo wa leo utakuwa mgumu.
Mara ya mwisho zilipokutana katika Kombe la Mapinduzi, Uwanja wa Amaan, Zanzibar mapema mwaka huu mechi ilitawaliwa na undava na Nahodha wa Azam, John Bocco aliondolewa uwanjani kwa kadi nyekundu timu hizo zikitoka 1-1.
Hall alimvaa Pluijm baada ya kipindi cha kwanza akataka kumchapa makofi, lakini baadaye akajutia uamuzi wake na kabla ya kuanza kipindi cha pili wakamaliza tofauti zao.
Yanga wanaingia uwanjani wakitokea kwenye kambi ya wiki moja kisiwani Pemba, wakati FC wanatokea makao makuu yao, Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Ni mechi ya mshike mshike mzito Yanga na Azam, wakati mwingine inafikia hata viongozi kununiana na mashabiki kuchapana makonde. Leo Taifa kazi ipo!
………………………………..
TANZANIA,
Twiga Stars imejiweka katika mazingira magumu ya kufuzu Fainali za Mataifa ya
Afrika kwa Wanawake baadaye mwaka huu Cameroon, baada ya kufungwa mabao 2-1
nyumbani na Zimbabwe jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es
Salaam.
Tanzania sasa itabidi ishinde ugenini kwa tofauti ya mabao mawili, au 2-1 ili mshindi aamuliwe kwa mikwaju ya penalti.
Katika mchezo wa leo uliohudhuriwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, Twiga Stars walianza vyema baada ya kutangulia kupata bao kupitia kwa kiungo wake mahiri, Mwanahamisi Omary ‘Gaucho’ dakika ya 17 kwa shuti kali la mbali baada ya kupokea pasi ya Asha Rashid ‘Mwalala’.
Tanzania sasa itabidi ishinde ugenini kwa tofauti ya mabao mawili, au 2-1 ili mshindi aamuliwe kwa mikwaju ya penalti.
Katika mchezo wa leo uliohudhuriwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, Twiga Stars walianza vyema baada ya kutangulia kupata bao kupitia kwa kiungo wake mahiri, Mwanahamisi Omary ‘Gaucho’ dakika ya 17 kwa shuti kali la mbali baada ya kupokea pasi ya Asha Rashid ‘Mwalala’.
Iliwachukua dakika mbili tu Zimbabwe kuchomoa bao hilo baada ya Erina Jeke kusawazisha kwa shuti la mbali dakika ya 19.
Mwanahimisi Gaucho alikaribia kufunga dakika ya 39 kama si shuti lake kutoka nje na dakika 45 za kwanza zilimalizika timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1.
Kipindi cha pili, Twiga Stars inayofundishwa na Nasra Juma ilirudi ikiwa dhaifu zaidi na kuwaruhusu wageni kutawala mchezo.
Zimbabwe ‘waliwakera’ mamia ya Watanzania waliojitokeza Uwanja wa Chamazi baada ya kupata bao la pili dakika ya kwanza tu ya kipindi cha pili, mfungaji Erina Jeke aliyefumua shuti akimalizia krosi ya Majory Nyauwe.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Fatuna Omary, Stumai Abdallah, Maimuna Khamis/Fatuna Khatib dk73, Fatuma Issa, Annastazia katunzi, Donisia Minja, Happinnes Mwaipaja, Amina BIlali, Shlder Boniphace/Fatuma Makusanya dk21, Asha Rashid ‘Mwalala’ na Mwanahamisi Omar ‘Gaucho’.
Zimbabwe; Chido Dzingirai, Felistus Muzingodi, Eunice Chibanda, Sheila makoto, Nobhule Majika, Luntet Mutokuto, Daisy Kaitano/Rejoice Kapfuvuti dk75, Emmaculate Msipa, Majory Nyauwe, Erina Jeke/Mavis Chirandu dk79 na Rudo Neshamba/Patience Mujuru dk90.
……………………………………………………….
KOCHA Mkuu wa Mbeya City FC, Mmalawi Kinnah Phiri
amesema kipa Juma Kaseja 'Baba Wawili' hatakuwamo kwenye programu ya mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Simba SC Jumapili hii kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam kutokana na sababu za kifamilia.
Muda mfupi uliopita kocha Phiri ameudokeza mtandao huu kuwa ilikuwa waungane na kipa huyo leo asubuhi kwenye kambi ya muda hapa Morogoro lakini imemlazimu kumuongezea muda zaidi wa kukaa karibu na familia yake ili kushughulikia masuala kadhaa ya kifamilia aliyonayo hivi sasa.
“Wakati anaondoka Mbeya siku tano zilizopita tulikubaliana kuwa ataungana nasi hapa siku ya leo, nimezungumza nae leo asubuhi kuna mambo muhimu ya kifamilia amenieleza hivyo basi nimeamua kumuongezea siku kadhaa za kubaki nyumbani kushughulikia yale yote yaliyopo kwenye familia yake na imani yangu kuwa ataungana na kikosi mara tu tutakaporejea mbeya kujiandaa na mchezo dhidi ya Stand United March 10.
Juma Kaseja aliondoka jijini Mbeya mara baada ya mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Tanzania Prison uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine kufuatia taarifa njema ya mkewe kujifungua watoto mapacha.
Wachezaji wanzeke na uongozi wa City kwa ujumla unampongeza Juma Kaseja na kumtakia kila la kheri kwenye malezi ya watoto wake.
Mbeya City imeweka kambi Morogoro kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba na inatarajiwa kuingia Dar es Salaam kesho.
Muda mfupi uliopita kocha Phiri ameudokeza mtandao huu kuwa ilikuwa waungane na kipa huyo leo asubuhi kwenye kambi ya muda hapa Morogoro lakini imemlazimu kumuongezea muda zaidi wa kukaa karibu na familia yake ili kushughulikia masuala kadhaa ya kifamilia aliyonayo hivi sasa.
“Wakati anaondoka Mbeya siku tano zilizopita tulikubaliana kuwa ataungana nasi hapa siku ya leo, nimezungumza nae leo asubuhi kuna mambo muhimu ya kifamilia amenieleza hivyo basi nimeamua kumuongezea siku kadhaa za kubaki nyumbani kushughulikia yale yote yaliyopo kwenye familia yake na imani yangu kuwa ataungana na kikosi mara tu tutakaporejea mbeya kujiandaa na mchezo dhidi ya Stand United March 10.
Juma Kaseja aliondoka jijini Mbeya mara baada ya mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Tanzania Prison uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine kufuatia taarifa njema ya mkewe kujifungua watoto mapacha.
Wachezaji wanzeke na uongozi wa City kwa ujumla unampongeza Juma Kaseja na kumtakia kila la kheri kwenye malezi ya watoto wake.
Mbeya City imeweka kambi Morogoro kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba na inatarajiwa kuingia Dar es Salaam kesho.
……………………………………………
KIUNGO wa Mbeya City, Ramadhani Chombo 'Redondo'
amesema historia itawabeba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
dhidi ya Simba Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Redondo amesema Mbeya City ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo kwa sababu imekuwa na historia nzuri kila inapokutana na Simba kwenye uwanja wa Taifa.
“City imeshinda mara kadhaa mbele ya Simba, hili ni jambo zuri kisaikolojia, kwa sababu linaleta kujiamini, imani yangu kubwa dakika 90 za Jumapili zitakuwa nzuri upande wetum” alisema.
Hata hivyo, kiungo huyo wa zamani wa Ashanti, Simba na Azam FC, amesema kwamba mchezo huo utakuwa mgumu kwa sababu timu zote zitakutana zikitoka kupoteza mechi zake zilizopita za Ligi Kuu.
“Ni wazi utakuwa mgumu, hii ni kwa sababu kila timu inahitaji matokeo mazuri baada ya kupoteza mchezo uliopita, Simba na timu nzuri na wako kwenye nafasi nzuri pia, lakini wasitegeme kupata ushindi kwa sababu sisi tunauhitaji zaidi yao,” alisema.
Redondo amesema Mbeya City ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo kwa sababu imekuwa na historia nzuri kila inapokutana na Simba kwenye uwanja wa Taifa.
“City imeshinda mara kadhaa mbele ya Simba, hili ni jambo zuri kisaikolojia, kwa sababu linaleta kujiamini, imani yangu kubwa dakika 90 za Jumapili zitakuwa nzuri upande wetum” alisema.
Hata hivyo, kiungo huyo wa zamani wa Ashanti, Simba na Azam FC, amesema kwamba mchezo huo utakuwa mgumu kwa sababu timu zote zitakutana zikitoka kupoteza mechi zake zilizopita za Ligi Kuu.
“Ni wazi utakuwa mgumu, hii ni kwa sababu kila timu inahitaji matokeo mazuri baada ya kupoteza mchezo uliopita, Simba na timu nzuri na wako kwenye nafasi nzuri pia, lakini wasitegeme kupata ushindi kwa sababu sisi tunauhitaji zaidi yao,” alisema.
…………………………..
HABARI
ZA KIBURUDANI.
WASANII wa muziki mbalimbali hapa nchini, Jumamosi hii
wanatarajiwa kukinukisha vilivyo katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini
Dar es Salaam, katika tamasha la Amsha Mama Festival. Akizungumza kwa niaba ya
wasanii wenzake, Balozi wa tamasha hilo Khalid Ramadhani ‘Tundaman’,
ambaye amepewa Ubalozi huo kupitia waandaaji wa tamasha la (AFWAB)
AMSHA MAMA Festival 2016, lililo chini ya Mkurugenzi Mtendaji wa lebo ya Candy
na Candy Records Joe Kariuki, alisema tamasha hilo linalotarajiwa
kufanyika Machi 5 mwaka huu katika uwanja wa Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.
Tundaman na Muandaaji wa tamasha hilo Kariuki, wamesema kwamba maandalizi ya
shoo hiyo tayari yameshakamilika kwa kiasi kikubwa hivyo angependa kutumia
fursa hii kuwaalika wakazi wote wa jiji la Dar, kujumuika siku hiyo kushuhudia
burudani mbalimbali zitakazotolewa na wasanii kibao ambao tayari wemedhibitisha
kufanya makamuzi siku hiyo. “Tunapenda kuwaalika Watanzania wote kwa ujumla
siku ya jumamosi hii ya Machi 5, mwaka huu waje kwa wingi katika Viwanja vya
Mwembe Yanga Temeke jijini Dar Salaam, ili tujumuike kwa pamoja katika
tamasha la kuhamasisha wanawake kujikwamua katika shughuli zao mbalimbali za
kiuchumi. Tamasha hili litakuwa ni la wazi kwa maana kwamba watu wote watapata
burudani kibao bila malipo yaani bure kabisa hivyo waje kuwashuhudia wasanii
kama, Khadija Kopa, Mr Blue, Snura, Msaga Sumu, Ali Chocky na Tunda Man wakitoa
burudani ya hali ya juu kwani ulinzi na usalama siku hiyo ni wa uhakika,”
alisema Tunda Man. Kwa upande wake, Joe Kariuki ambaye ni mratibu mkuu wa
tamasha hilo ametumia muda huu kuongea na baadhi ya akinamama wanaojishughulisha
na biashara za vitu mbalimbali hususani mama ntilie, wauza matunda na wauzaji
wa mitumba ili nao wajitokeze kwa wingi kuja kunadi bidhaa zao siku hiyo
kwani hiyo ndiyo fursa yao ya kipekee ya kujitangaza bure.
…………………………………….
…………………………………….
Mama mzazi wa Banza Stone Bi Hadija au Sozi alizikwa jijini
Dar es Salaam kwenye makaburi ya Sinza jirani kabisa. Mama huyo akazikwa jirani
kabisa na kaburi la mwanae - Banza Stone aliyefariki mwaka jana. Mazishi ya
mama wa Banza yalikwenda sambamba na ya mjukuu wake au wajina wake Sozi Masanja
ambaye ambaye ni mtoto wa dada yake Banza. Mama wa mjukuu huyo alishafariki
kiasi cha miaka sita iliyopita. Mjukuu huyo wa mama yake Banza mwenye umri wa
miaka 45 amekuwa akichukuliwa na majirani wengi kama mtoto wa mama yake Banza
hali iliyoleta mchanganyiko kwa wengi wakati wa kuripoti vifo vyao. Mjukuu huyo
aliyeacha watoto wawili alifariki juzi asubuhi akiwa njiani kupelekwa hospitali
baada ya kuzidiwa na mmoja wa watu walioshiriki kumwingiza kwenye gari kwa
safari ya kuwahishwa hospitali ni mama yake Banza. Masaa wawili baada ya kifo
cha mjukuu wake, mama wa Banza nae akafariki kwa msongo wa mawazo
……………………………………..
……………………………………..
STAA wa kike wa muvi za Kibongo, Kajala Masanja amesema
kwamba mambo ya kimjini kama wafanyavyo mastaa wengine, kwa sasa ameyapa mgongo
kwa madai kuwa anaona anaelekea uzeeni. Akiongea na Saluti5, Kajala alisema
kwamba kila akijiangalia anaona kabisa kuwa alivyokuwa zamani sio alivyo sasa
hivyo ana kila sababu ya kubadilika na kuwa na utulivu. “Kiukweli najiona
kabisa naelekea uzeeni, ule usichana unapotea na hivyo ni vyema sasa mambo
mengine ya kimjini nikayapa kisogo,” alisema Kajala. “Kwenda klabu usiku
nimepunguza na kuna siku nitaacha kabisa, nguo za ajabuajabu najifikiria mara
mbilimbili kuzitia mwilini,” aliongeza staa huyo.
…………………………………………..
…………………………………………..
MKALI wa Bongofleva, Baraka da Prince amemkana laivu staa
wa filamu, Nisha akisema kuwa hajawahi kuwa na uhusiano nae wa kimapenzi.
Katika mahojiano na kipindi cha E – News cha runinga ya EATV, Baraka da Prince
aliulizwa kwa mafumbo kama ana uhusianao na msanii huyo (hakutajwa jina). Kabla
hajakana, Baraka da Prince kwanza alijifanya kutomfahamu msanii anayehusishwa
naye, ambapo baada ya sekunde kadhaa ndipo alipojifanya kumkumbuka na kusema:
“Ahaaa… Nisha sio? Hapana mi sijawahi ku date na yule dada,” alisema Baraka
anayetikisa anga la Bongofleva kwa nyimbo zake nyingi kali.
HABARI ZA MICHEZO KIMATAIFA.
BARCELONA imezidi kukimbia
kivuli chake katika Ligi Kuu ya Hispania, maarufu kama La Liga baada ya ushindi
wa mabao 5-1 usiku huu dhidi ya wenyeji Rayo Vallecano Uwanja wa Rayo Vallecano
mjini Madrid.
Mwanasoka bora kabisa kuwahi kutokea duniani, Lionel Messi amefunga mabao matatu peke yake usiku huu katika dakika za 23, 53 na 72, huku mabao mengine ya Barca yakifungwa na Ivan Rakitic dakika ya 22 na Arda Turan dakika ya 86.
Mwanasoka bora kabisa kuwahi kutokea duniani, Lionel Messi amefunga mabao matatu peke yake usiku huu katika dakika za 23, 53 na 72, huku mabao mengine ya Barca yakifungwa na Ivan Rakitic dakika ya 22 na Arda Turan dakika ya 86.
Bao pekee Rayo Vallecano limefungwa na
mshambuliaji wa kimataifa wa Angola, Manucho Goncalves dakika ya 57 na
sasa Barca inafikisha pointi 66 baada ya kucheza mechi 26 na kuendelea
kujinafasi kileleni mwa La Liga, ikifuatiwa na Atletico Madrid yenye
pointi 61 za mechi 27 na Real Madrid yenye pointi 57 za mechi 27 pia.
Rayo Vallecano inabaki na pointi zake 26 za mechi 26 na kuendelea kushika nafasi ya 16 katika ligi ya timu za 20.
Katika mchezo huo, Rayo iliwapoteza wachezaji wake wawili waliotolewa kwa kadi nyekundu, Diego Llorente aliyemchezea vibaya Rakitic dakika ya na Manuel Iturra aliyemuangusha Luis Suarez kwenye boksi. Lakini Suarez alikosa penalti iliyotolewa baada ya kuangushwa kwake.
Rayo Vallecano inabaki na pointi zake 26 za mechi 26 na kuendelea kushika nafasi ya 16 katika ligi ya timu za 20.
Katika mchezo huo, Rayo iliwapoteza wachezaji wake wawili waliotolewa kwa kadi nyekundu, Diego Llorente aliyemchezea vibaya Rakitic dakika ya na Manuel Iturra aliyemuangusha Luis Suarez kwenye boksi. Lakini Suarez alikosa penalti iliyotolewa baada ya kuangushwa kwake.
…………………………………
TIMU ya Liverpool imeichapa
mabao 3-0 Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku huu Uwanja
wa Anfiled.
Ushindi huo ni sawa na kisasi cha kufungwa kwa penalti 3-1 katika fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup Februari 28, Uwanja wa Wembley baada ya sare ya 1-1.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Liverpool yamefungwa na Adam Lallana dakika ya 34, James Milner dakika ya 41 na Roberto Firmino dakika ya 57.
Ushindi huo ni sawa na kisasi cha kufungwa kwa penalti 3-1 katika fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup Februari 28, Uwanja wa Wembley baada ya sare ya 1-1.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Liverpool yamefungwa na Adam Lallana dakika ya 34, James Milner dakika ya 41 na Roberto Firmino dakika ya 57.
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya England usiku huu, Manchester United imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga 1-0 Watford, bao pekee la Juan Mata dakika ya 83 Uwanja wa Old Trafford.
Arsenal imefungwa 2-1 nyumbani na Swansea City Uwanja wa Emirates katika mchezo mwigine wa ligi hiyo. Mabao ya Swansea yamefungwa na Wayne Routledge dakika ya 32 na Ashley Williams dakika ya 74, wakati la Gunners limefungwa na Joel Campbell dakika ya 15.
Stoke City imeilaza 1-0 Newcastle United, bao pekee la Xherdan Shaqiri dakika y 80 Uwanja wa Britannia.
West Ham United imeilaza 1-0 Tottenham Hotspur, bao pekee la Michail Antonio dakika ya saba.
………………………………..
BEKI
wa kimataifa wa Ivory Coast, Emmanuel Eboue anaweza kurejea Ligi Kuu ya
England, baada ya klabu ya Sunderland kuonyesha nia ya kumsajili.
Beki
huyo wa zamani wa Arsenal amekuwa kivutio kwenye mazoezi ya Sunderland na leo
anatarajiwa kusaini Mkataba wa hadi mwishoni mwa msimu.
Mkongwe
huyo mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa ni mchezaji huyu baada ya kutemwa na
klabu ya Galatasaray mwaka jana. Kwa wiki tatu amekuwa akifanya mazoezi na
Sunderland na akacheza dakika zote 90 Jumatatu U21 ya klabu hiyo ikiifunga
Leicester City.
WASIFU WA EMMANUEL EBOUE
Mwaka
Timu Mechi Mabao
2001–2002
ASEC 25- (3)
2002–2005
Beveren 70- (4)
2005–2011
Arsenal 132-(5)
2011–2015
G'tasaray 77-(4)
Kocha
Sam Allardyce aliuangalia mchezo huo wakati kocha wa U21, Andy Welsh alivutiwa
na mchango wa mchezaji huyo wa Ivory Coast.
"Nilizungumza
naye na alisema hizo zilikuwa dakika 90 za kwanza kucheza kwa zaidi ya
mwaka," amesema Welsh.
"Alionyesha
juhudi nzuri na alionekana vizuri wakati mchezo ukiwa mkali. Amekuwa mtu mzuri
kwenye chumba cha kubadilishia nguo akiwa na wachezaji nyota Chipukizi,
anawasaidia, hivyo sijapata malalamiko yoyote.
……………………….
SHIRIKISHO la Soka Rwanda
(FERWAFA) iatsaini mkataba wa muda mredu na klabu ya Feyenoord ya Uholanzi kwa
ajili ya maendeleo ya soka Rwanda.
Rais wa FERWAFA, Vincent Degaule Nzamwita amekutaka na Meneja Uhusiano wa Kimataifa wa klabu hiyo, Gido Vader Jumanne kukamilisha mipango kwa ajili ya akademi ya vijana nchini Rwanda.
Balozi wa Rwanda nchini Uholanzi, Jean Pierre Karabaranga pia alihudhuria mkutano huo, makao makuu ya klabu hiyo mjini Rotterdam.
“Mkutano ulilenga kuangalia uwezekano kuyafanyia kazi yale ambayo tuliyajadili katika mikutano yetu ya awali na kipi kinahitajika ili kuimarisha uhusiano wetu na Feyenoord,” amesema Nzamwita.
Rais wa FERWAFA, Vincent Degaule Nzamwita amekutaka na Meneja Uhusiano wa Kimataifa wa klabu hiyo, Gido Vader Jumanne kukamilisha mipango kwa ajili ya akademi ya vijana nchini Rwanda.
Balozi wa Rwanda nchini Uholanzi, Jean Pierre Karabaranga pia alihudhuria mkutano huo, makao makuu ya klabu hiyo mjini Rotterdam.
“Mkutano ulilenga kuangalia uwezekano kuyafanyia kazi yale ambayo tuliyajadili katika mikutano yetu ya awali na kipi kinahitajika ili kuimarisha uhusiano wetu na Feyenoord,” amesema Nzamwita.
“Tangu tumepanga kuwa na mashindano ya U-15, msaada wao wa kiufundi utakuwa muhimu sana sana kukuza skka yetu nchini. Tunaamini muda si mrefu tutaanza kunufaika na msaada wao wa kiufundi. Pia tunamhsukuru Balozi Karabaranga kwa msaada wake kuhakikisha kwamba Feyenoord inakuja kusaidia kuendeleza sekta ya soka,” amesema.
Mwaka jana FERWAFA ilinzisha mashindano ya ligi za vijana chini ya umri wa miaka 15 na miaka 13 (U-15 na U-13) kwa wote, wasichana na wavulana.
Na mabingwa mara 14 wa Ligi ya Uholanzi, maarufu kama Eredivisie wanasifika kwa kuzalisha wachezaji nyota duniani kama Robin Van Persie ambaye kwa sasa anachezea Fenerbahce ya Uturuki baada ya kuwika Arsenal na Manchester United za Ligi Kuu ya England.
Wengine ni Giovanni van Brockhorst, Johan Cruyff, Ruud Gullit, Dirk Kuyt, Bruno Martins Indi na Ron Vlaar.
Akademi ya vijana ya Feyenoord pia ina uhusiano na nchi za Ghana, Nigeria, Afrka Kusini na Vietnam.
Akademi ya Feyenoord inayojulikana kama Varkenoord, ina mfumo mzuri unaoheshimika nchini Uholanzi ambayo imeshinda tuzo ya Rinus Michels kama akademi bora ya vijana kwa miaka mitano mfululizo tangu mwaka 2009.
Varkenoord ilitoa wachezaji 11 katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil, ambayo ni idadi kubwa kuliko akademi zote duniani.
…………………………….
MABINGWA
wa Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wataanza
kutetea taji lao kwa kumenyana na St George ya Ethiopia katika hatua ya timu 32
Bora.
Timu hiyo ya mshambuliaji wa Tanzania, Thomas Ulimwengu itaanzia ugenini Machi 11, mwaka huu kabla ya kurudiana mjini Lubumbashi, wiki moja baadaye.
Timu hiyo ya mshambuliaji wa Tanzania, Thomas Ulimwengu itaanzia ugenini Machi 11, mwaka huu kabla ya kurudiana mjini Lubumbashi, wiki moja baadaye.
RATIBA KAMILI 32 BORA LIGI YA MABINGWA
AFRIKA .
Warri Wolves
|
v
|
El Merreikh
|
TBC
|
|||
Olympique Khouribga
|
v
|
ES Sahel
|
TBC
|
|||
Stade Malien
|
v
|
Coton Sport FC
|
TBC
|
|||
US Douala
|
v
|
Zamalek
|
TBC
|
|||
AS Vita Club
|
v
|
Clube Ferroviário de Maputo
|
TBC
|
|||
APR FC
|
v
|
Young Africans
|
TBC
|
|||
St. George
|
v
|
TP Mazembe
|
TBC
|
|||
Jumapili Machi 13, 2016
|
||||||
Mamelodi Sundowns
|
v
|
AC Leopards
|
TBC
|
||
Zesco United
|
v
|
Horoya A.C
|
TBC
|
||
Club Africain
|
v
|
MO Béjaïa
|
TBC
|
||
Etoile du Congo
|
v
|
ES Setif
|
TBC
|
||
Recreativo do Libolo
|
v
|
Al Ahly
|
TBC
|
||
Ahly Tripoli
|
v
|
El Hilal
|
………………………….
KLABU ya
Liverpool imebainisha azma yake ya kusainisha wafumania nyavu walio na uwezo na
sasa wanamuhitaji Edin Dzeko anayekipiga AS Roma kwa mkopo akitokea Manchester
City. Hatua hiyo ya kocha wa sasa wa majogoo hao wa jiji, Jurgen Klopp inakuja
siku chache baada ya kukiri anahitaji kuona anapata straika wa kuwasaidia akina
Divock Origin a Christian Benteke. Katika nia hiyo ya kusuka idara ya
ufumaniaji nyavu, bosi huyo wa majogoo wa jiji yumo katika mbio za kumwania pia
Danny Ings wa Burnley. Dzeko anadaiwa kuwaniwa pia na mabingwa wa zamani wa
England, Chelsea. Lakini hata hivyo, kwa taratibu za masuala ya uhamisho, Dzeko
anaweza kuhama kwa kukubaliana baina ya klabu yake na timu inayohitaji mchango
wake ambako dau la kumng’oa limetajwa kufikia pauni mil. 25. Taarifa za ndani
ya Liverpool zinasema kuwa Klopp yumo katika mpango wa kuwatema jumla ama kwa
mkopo baadhi ya wanandinga wake.
……………………………………………………………………………….
……………………………………………………………………………….
KLABU ya
Manchester United wameendelea kuichokoza tena Real Madrid na sasa wamepania
tena kupata saini ya Gareth Bale. Taarifa za ndani ya Klabu ya Manchester
United zinasema kuwa bosi wao, Louis Van Gaal amepewa ridhaa na uongozi kwa
ajili ya kumsajili Bale kwa gharama ambayo haikutajwa. Mpango wa mwaka huu
Manchester United ni kama wanakumbusha kidonda cha mwaka jana ambapo klabu hizo
mbili ziliingia vitani kwa kila moja kuhitaji mchezaji wa upande wa pili.
Katika harakati hizo, united walikuwa wanamwania beki Sargio Ramos ambapo
Madrid walikuwa wakisaka saini ya mlinda mlango wa United, David de Gea.
Mwishoni mwa msimu uliopita, magazeti ya michezo nchini Hispania, likiwemo
Marca liliandika taarifa za awali za Real Madrid kumtengea dau david de Gea
kiasi cha pauni 28.6 huku ikisema kuwa bado wana nafasi ya kufika bei
wanayoitaka United. Pamoja na De Gea, pia vigogo hao wa La Liga walikuwa
wanahitaji pia saini ya mlinzi wa timu ya taifa ya Ureno, Fabio Coentrao.
Wakisikiliza tetesi hizo, Manchester United wamweka mezani dau la pauni mil. 29
na bila shaka wamewalenga Real Madrid.
………………………………………………………….
………………………………………………………….
KLABU za jiji
la Manchester za Manchester United na Manchester City zimejikuta zikichuana
kuwania saini ya nyota wa Juventus ya Italia, Alex Sandro. Hata hivyo maombi ya
klabu zote hizo ya kumtwaa mchezaji huyo anayetesa katika Ligi ya Italia ya
serie A, yamekataliwa kwa mujibu wa Calcio Melcato.
…………………………………………………………………..
…………………………………………………………………..
NYOTA Pablo
Zabaleta amesema kwamba anavyoamini Manchester City inaweza kutumia uzoefu wake
na kuzinduka na kisha ikatwaa ubingwa wa michuano ya Ligi Kuu England. Man City
ilitwaa taji lake la kwanza msimu huu Jumapili kwa kuichapa Liverpool kwa
mikwaju ya penati na kufanikiwa kutwaa Kombe la Ligi baada ya timu hizo
kufungana bao 1-1 mtanange uliopigwa kwenye uwanja wa Wembley. Miamba hiyo
inautana tena leo kwenye uwanja wa Anfield huku Man City waiwa nyuma kwa pointi
tisa baada ya kufungwa na timu zinazoongoza Ligi hiyo, Leicester City na
Tottenham katika mechi zake mbili ilizokutana nazo. Hata hivyo Zabaleta anaamini
kwa sasa mirari wao upo juu kutokana na ushindi wa mabao 3-1 walioupata
Jumatano dhidi ya Dynamo Kiev katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya na taji
hilo la Wembley. Mbali na hilo, Muargentina huyo anakumbushia Man City
walivyotwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu wa 2011/12 licha ya kuwa ilikuwa nyuma
kwa pointi nane dhidi ya Manchester United huku zikiwa zimebaki mechi sita na
jinsi ilivyozinduka wiki za mwisho na kuipindua Liverpool kutoka kileleni mwa
Ligi msimu wa 2013/14. “Bado kuna pointi 36 za kushindania katika michuano ya
Ligi Kuu ambazo ni mechi nyingi,” Zabaleta alisema wakati akinukuliwa na gazeti
la Manchester Evening News. “Miaka michache iliyopita tuliwahi kuwa katika hali
kama hii. Tulipotwaa ubingwa wa Ligi kama hii tulikuwa nyuma kwa pointi nane
dhidi ya timu zilizokuwa zikiongoza na sasa bado tuna mechi mkononi,”
aliongeza. Alisema kuwa katika kipindi hiki ni kuelekeza nguvu zao kwenye
michuano hiyo ya Ligi Kuu na wajaribu kushinda mechi yao ya leo.
…………………………………………………………….
…………………………………………………………….
STAA wa timu
ya New York City, Andrea Pirlo ameshindwa kukataa kuwapo kwa uwezekano wa
kuongeza mkataba wake na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Marekani (MLS). Mkataba wa
sasa wa Pirlo unamalizika Desemba mwaka huu, baada ya kiungo huyo wa timu ya
taifa ya Italia kuungana na nyota wenzake, David Villa na Frank Lampard
akitokea Juventus mwaka jana. Kwa sasa nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 yupo
katika dakika zake za mwisho katika kibarua chake, lakini Pirlo anafurahia
maisha ya jijini New York na ameshaonekana wazi kuna uwezekano wa kuendelea
kuchezea klabu hiyo inayotumia uwanja wa Yankee. “Siwezi kukataa mawazo ya
kuendelea kubaki mahali hapa,” Pirlo aliliambia gazeti la New York Times. “Hiki
ni kitu ambacho kinaweza kuvutia kutokana na kwamba mara zote nimekuwa
nikipenda kuja hapa kucheza, lakini sijawahi kuwaza kama ingekuwa hivi
karibuni,” aliongeza staa huyo.
………………………………………………………
………………………………………………………
BEKI wa
Liverpool, Kolo Toure anaamini Ligi ya Europe inaweza akuiokoa timu yake baada
ya kupoteza mechi ya Kombe la Capital One. Kikosi hicho cha jurgen Klopp
kilitunguliwa na Manchester City kwa mikwaju ya penati na kupoteza nafasi nzuri
ya kunyanyua Kombe msimu huu. Wakiwa katika nafasi ya tisa Ligi Kuu, Liverpool
watawakabili Manchester United katika timu 16 za mwisho Ligi ya Europe. Toure,
34, anahisi Ligi ya Europe itakuwa tumaini kwa Liverpool msimu huu wa 2015/16.
“Tunaweza kumaliza msimu wetu vizuri kwa kushinda Kombe la Europe ingawa Ligi
ya Uingereza bado haijaisha,” alisema. “Tuna mechi nyingi mbele yetu.
Tuna mechi nyingine muhimu zaidi. Tunahitaji kusahau kipigo cha City ili tuweze
kuendelea na majukumu mengine,” aliongeza.
………………………………………………………………..
………………………………………………………………..
NI kama vile
kamchongea, nyota wa zamani wa Arsenal, Paul Merson amesema kwamba kocha Arsene
Wenger ni lazima afukuzwe endapo timu za Leicester City ama Tottenham
zitashinda katika mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu England. Arsenal ambayo
haijawahi kutwaa ubingwa wa michuano hiyo tangu mwaka 2004, kwa sasa ipo nyuma
ya pointi tano dhidi ya Leicester City kutokana na kipigo cha Jumapili cha
mabao 3-2 kutoka kwa majeruhi Manchester United, huku Spurs wao wakiwa wamebaki
nyuma kwa pointi mbili dhidi ya vijana hao wa Claudio Ranieri baada ya kupata
ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya vinara hao. Vijana hao wa Wenger baadae
leo wanakutana na Swansea kabla ya kucheza ‘derby’ kali ya jiji la London dhidi
ya Spurs na Merson ambaye aliwahi kucheza chini ya Mfaransa huyo msimu wa
1996-97, anasema kwamba anavyodhani kocha huyo mwenye umri wa miaka 66 na
ambaye ameinoa klabu hiyo kwa muda wa miaka 20, anatakiwa kuachia nmgazi endapo
timu hiyo itashindwa tena mwaka huu kutwaa ubingwa mbele ya washindani wake
hao.
……………………………………………………………………
……………………………………………………………………
MECHI ZA LEO KATIKA LIGI MBALIMBALI ZILIZOCHEZWA
NA ZA LEO.
ENGLAND.
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
……………………………………………..
HISPANIA.
02/03
|
|||
02/03
|
|||
03/03
|
|||
03/03
|
|||
03/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
05/03
|
|||
06/03
|
……………………………………………..
UJERUMANI.
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
|||
02/03
|
Borussia dotmund
|
||
05/03
|
Schalke 04
|
||
05/03
|
IngolstaDAT
|
||
05/03
|
Hannover 96
|
||
05/03
|
Bayer Leverkusen
|
||
05/03
|
MSIMAMO
WA LIGI MBALI MBALI.
HISPANIA.
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
…………………………………………………
German Bundesliga | LOGS
……………………………………………………….
English Barclays
Premier League | LOGS
…………………………………………………..
|
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
Juventus
|
27
|
19
|
4
|
4
|
48
|
15
|
33
|
61
|
2
|
Napoli
|
27
|
17
|
7
|
3
|
55
|
22
|
33
|
58
|
3
|
Roma
|
28
|
16
|
8
|
4
|
59
|
29
|
30
|
56
|
4
|
Fiorentina
|
28
|
16
|
5
|
7
|
49
|
31
|
18
|
53
|
5
|
Internazionale
|
27
|
14
|
6
|
7
|
34
|
25
|
9
|
48
|
6
|
Milan
|
27
|
13
|
8
|
6
|
39
|
28
|
11
|
47
|
7
|
Sassuolo
|
27
|
10
|
11
|
6
|
34
|
31
|
3
|
41
|
8
|
Lazio
|
27
|
10
|
7
|
10
|
34
|
36
|
-2
|
37
|
9
|
Bologna
|
27
|
10
|
5
|
12
|
29
|
31
|
-2
|
35
|
10
|
Chievo
|
27
|
9
|
7
|
11
|
32
|
36
|
-4
|
34
|
11
|
Empoli
|
27
|
9
|
7
|
11
|
33
|
40
|
-7
|
34
|
12
|
Torino
|
27
|
8
|
8
|
11
|
33
|
34
|
-1
|
32
|
13
|
Atalanta
|
27
|
7
|
9
|
11
|
26
|
31
|
-5
|
30
|
14
|
Udinese
|
27
|
8
|
6
|
13
|
24
|
40
|
-16
|
30
|
15
|
Genoa
|
27
|
7
|
7
|
13
|
27
|
32
|
-5
|
28
|
16
|
Sampdoria
|
27
|
7
|
7
|
13
|
39
|
46
|
-7
|
28
|
17
|
Palermo
|
27
|
7
|
6
|
14
|
27
|
47
|
20
|
27
|
18
|
Frosinone
|
27
|
6
|
5
|
16
|
26
|
53
|
27
|
23
|
19
|
Carpi
|
27
|
4
|
9
|
14
|
24
|
44
|
20
|
21
|
20
|
Verona
|
27
|
2
|
12
|
13
|
24
|
45
|
21
|
18
|
………………………………………
French Ligue 1 | LOGS
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
Paris Saint-Germain
|
28
|
23
|
4
|
1
|
68
|
15
|
53
|
73
|
2
|
Monaco
|
29
|
13
|
12
|
4
|
42
|
32
|
10
|
51
|
3
|
Caen
|
29
|
13
|
4
|
12
|
32
|
38
|
-6
|
43
|
4
|
Lyon
|
28
|
12
|
6
|
10
|
40
|
30
|
10
|
42
|
5
|
Nice
|
28
|
11
|
8
|
9
|
39
|
32
|
7
|
41
|
6
|
Rennes
|
28
|
10
|
11
|
7
|
36
|
33
|
3
|
41
|
7
|
St Etienne
|
28
|
12
|
5
|
11
|
33
|
32
|
1
|
41
|
8
|
Nantes
|
27
|
10
|
10
|
7
|
26
|
24
|
2
|
40
|
9
|
Angers
|
28
|
10
|
8
|
10
|
29
|
29
|
0
|
38
|
10
|
Lorient
|
28
|
9
|
10
|
9
|
40
|
41
|
-1
|
37
|
11
|
Bastia
|
27
|
11
|
4
|
12
|
27
|
29
|
-2
|
37
|
12
|
Bordeaux
|
28
|
9
|
10
|
9
|
37
|
43
|
-6
|
37
|
13
|
Marseille
|
27
|
8
|
12
|
7
|
37
|
28
|
9
|
36
|
14
|
Montpellier
|
28
|
10
|
5
|
13
|
36
|
33
|
3
|
35
|
15
|
Lille
|
28
|
7
|
13
|
8
|
21
|
23
|
-2
|
34
|
16
|
Guingamp
|
28
|
8
|
8
|
12
|
33
|
40
|
-7
|
32
|
17
|
Reims
|
28
|
8
|
8
|
12
|
32
|
39
|
-7
|
32
|
18
|
GFC Ajaccio
|
27
|
6
|
10
|
11
|
28
|
38
|
10
|
28
|
19
|
Toulouse
|
28
|
4
|
10
|
14
|
27
|
47
|
20
|
22
|
20
|
Troyes
|
28
|
2
|
8
|
18
|
20
|
57
|
37
|
14
|
MWISHOOOOOOOOOO.