Video Information
MAKALA YA
MICHEZO NA BURUDANI
……..MUKHTASARI
WAKE……..
- Kazi ipo
Uwanja wa Taifa kesho Jumapili wakati Yanga itakapoivaa Friends Rangers katika
michuano ya Azam Sports au Kombe la FA.
- Kiungo kinda wa Simba, Said Ndemla, anatarajia kwenda kufanya
majaribio kwenye kikosi cha TP Mazembe ya DR Congo ili kusaka nafasi ya kucheza
soka katika klabu hiyo.
- Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
ametuma salamu za rambi rambi kwa klabu ya Tanzania Prisons inayoshiriki Ligi
Kuu ya Vodacom kufuatia kifo cha Mwenyekiti wake Hassan Mlilo kilichotokea katika hospital ya Taifa ya Muhimbili jijini
Dar es Salaam.
KIMATAIFA.
- Manchester United wamekanusha habari kwamba walikutana na
kuzungumza na meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola.
HABARI
KAMILI ZA KIMICHEZO.
Kazi ipo Uwanja wa Taifa kesho Jumapili wakati Yanga itakapoivaa
Friends Rangers katika michuano ya Azam Sports au Kombe la FA.
Friends Rangers timu ya Ligi Daraja la Kwanza, imepanga kuwatumia mastraika
wake hatari ambao wamewahi kucheza katika klabu za Sweden na Dubai ili
kuhakikisha wanashinda mechi hiyo.
Kocha wa Friends Rangers, Herry Mzozo, alisema atamtumia
straika, Juma Mgaya ambaye amewahi kucheza nchini Sweden na Cosmas Lewis
‘Balotelli’ aliyewahi kucheza Dubai.
“Hao Yanga ni timu kongwe tu na siyo timu ya kututisha
sisi, tuna mikakati yetu ya kuhakikisha tunashinda, ndiyo maana tunao hao
wachezaji,” alisema Mzozo.
Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi, alisema: “Tumejiandaa
vizuri kwa mechi hii, labda niseme wazi tu kwamba tutatumia kikosi cha pili kwa
lengo la kupumzisha wachezaji wetu.”
Katika michuano hiyo, leo Jumamosi Simba itacheza na Burkina
Faso kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakati jijini Mwanza, Pamba itacheza na
Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.
Mjini Mtwara kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Ndanda FC
itacheza na Mshikamano FC. Mechi nyingine za kesho Jumapili, Njombe Mji
itacheza na Prisons kwenye Uwanja wa Amani, Njombe na Stand United itaivaa
Mwadui FC kwenye Uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga.
…………………………………………………..
Kiungo kinda wa Simba, Said Ndemla, anatarajia kwenda kufanya
majaribio kwenye kikosi cha TP Mazembe ya DR Congo ili kusaka nafasi ya kucheza
soka katika klabu hiyo.
Hivi karibuni, Watanzania, Abuu Ubwa na Haruna Chanongo walienda
kufanya majaribio Mazembe ambapo kwa sasa hatua iliyobaki ni makubaliano kati
yao na Stand United inayowamiliki wachezaji hao.
Jamali Kisongo ambaye ni meneja wa Mbwana Samatta,
amesema kuwa, ataendelea kuwasaidia wachezaji wa Tanzania kupenya kwenye
soka la kimataifa kama Samatta.
“Nimewapeleka Ubwa na Chanongo kufanya majaribio TP Mazembe,
kinachoendelea sasa ni mazungumzo kati ya Stand na Mazembe kwa ajili ya
usajili.
“Ndemla naye nitampeleka akafanye majaribio kule, lengo ni kuwasaidia
wachezaji wengi wa hapa nyumbani kupata fursa ya kucheza soka nje ya mipaka ya
nchi yetu.
“Mbali na Ndemla, pia kiungo wa Mtibwa (Sugar), Mohammed
Ibrahim, naye anahitajika kule baada ya awali safari yake kushindikana,”
alisema Kisongo.
………………………………………………………………
Hii ndiyo habari ya mjini pale mjini Shinyanga, kwmaba straika
Elias Maguri wa Stand United hana nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu yake
jambo linalompa ugumu kupambana na Amissi Tambwe wa Yanga kuwania ufungaji
bora.
Katika Ligi Kuu Bara hadi sasa, Tambwe anaongoza kwa ufungaji
akiwa na mabao 13, akifuatiwa na Hamis Kiiza wa Simba mwenye mabao 10 huku
Maguri akiwa na mabao tisa sawa na Donald Ngoma wa Yanga.
Maguri amepoteza nafasi kikosi cha kwanza baada ya kuvurugana na
kocha wake, Patrick Liewig siku chache baada ya kung’ara na kikosi cha Taifa
Stars na Kilimanjaro Stars.
Taifa Stars ilipocheza dhidi ya Algeria mwaka jana kuwania
kufuzu Kombe la Dunia 2018, Maguri aliifungia Stars bao moja katika sare ya
mabao 2-2 jijini Dar es Salaam.
Maguri alisema; “Sina nafasi kikosi cha kwanza, hivyo siwezi
tena kuwania tuzo ya mfungaji bora na nawaachia vita hiyo, Tambwe na Kiiza.
“Kocha hataki kunipanga kwa sababu eti mimi ni staa na yeye
hataki mchezaji staa katika kikosi chake jambo ambalo siyo kweli, Tambwe na
Kiiza wao wana nafasi katika vikosi vyao, hivyo wanaweza kufanya vizuri.”
Alipotafutwa Liewig, alisema; “Mtu hajitumi nimpe nafasi ili
iweje? Tangu aliporudi amekuwa wa kawaida mno kikosini.”
…………………………………………………………………..
Uongozi wa klabu ya Friends Rangers, umesema
klabu ya Yanga isitarajie mteremko katika mchezo wao wa kutania Kombe
la FA, utakaofanyika keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es
Salaam.
Ofisa habari wa klabu hiyo Asha Kigundula,
amesema licha ya kujua wanacheza na timu inayoongoza Ligi Kuu,
wao wamejipanga kushinda mchezo huo.
"Kikosi chetu kipo kambini na kila kitu
kinakwenda vizuri kabisa kwa ajili ya kujiandaa na mechi hiyo ya Jumapili.
"Kikubwa nilitaka kuwatahadharisha Yanga,
wasitarajie mteremko eti kwa kuwa wanakuja kucheza na Friends Rangers. Tuko
vizuri na tutawashangaza," alisema Kigundula akionyesha imani kubwa na
kikosi chake.
Kigundula alisema Yanga isiifananishe timu yao na
timu iliyoifunga mabao 5-0, hivyo kwao wanakuja kamili kuhakikisha
wanaitoa na kuendelea katika hatua inayoufuata.
"Tumejipanga kushinda hivyo Yanga ifute
ndoto za kutufunga kwa sababu juzi ilipata ushindi wa mabao mengi,
wameifunga timu ambayo ilipanda kizengwe wasubili
waone tutakachowafanya"alisema Kigundula
Hata hivyo Kigundula amewataka mashabiki wa timu
hiyo wajitokeze kwa wingi katika mchezo wao ili waweze kuwapa hali
zaidi wachezaji wao wacheze kwa kujiamini.
……………………………………………………….
Kikao cha Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini (TFF) kilichoketi jana na kupitia taarifa mbalimbali za michezo ya Kombe
la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mzunguko wa pili, kimeiondoa klabu
ya Ashanti United kwenye michuano hiyo na nafasi yake kuchukuliwa na klabu ya
Africa Lyon.
Katika kikao hicho kamati ilipokea malalamiko ya klabu ya Africa
Lyon dhidi ya Ashanti United kwa kumchezesha mchezaji Enock Balagashi kwa jina
la Awesu Abdu katika mchezo namba 3, uliochezwa tarehe 15 Disemba, 2015 na
Ashanti kuibuka na ushindi kwa mikwaju ya penati.
Kamati imejiridhisha baada ya kupitia taarifa ya mchezo huo, na
kubaini klabu ya Ashanti United ilifanya udanganyifu wa kumtumia mchezji huyo
kwa jina la mchezaji mwingine, huku ikitambua kuwa kufanya hivyo ni makosa na
mchezo huo ulikuwa ukionyeshwa moja kwa moja kwenye kituo cha luninga cha
Azamtv.
Kwa mujibu wa Kanuni no. 41 (12) ya uthibiti wa viongozi
kufungiwa miezi 12, Kamati imemfungia Katibu Mkuu wa klabu ya Ashanti
kutojihusisha na masuala ya mpira wa miguu kwa kipindi cha miezi 12.
Aidha Kamati pia kwa kutumia kanuni ya 37 (15) ya udhibiti wa
wachezaji, mchezaji Enock Balagashi amefungiwa kwa kucheza mpira kwa kipindi ch
amiezi 12 na faini ya shilingi laki tatu (300,000).
Kamati imevitaka vilabu vya ngazi zote nchini kuheshimu vipindi
vya usajili kwa kufanya usajili wa wachezaji watakaowatumia, na kuheshimu
kanuni na taratibu zinazoendesha michuano inayoandaliwa na TFF.
Africa Lyon watacheza dhidi ya Azam FC mznguko wa tatu siku ya
Jumatatu katika Uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………….
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma
salamu za rambi rambi kwa klabu ya Tanzania Prisons inayoshiriki Ligi Kuu ya
Vodacom kufuatia kifo cha Mwenyekiti wake Hassan Mlilo kilichotokea jana katika
hospital ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Katika salamu zake, Malinzi amewapa pole familia ya marehemu
Hassan Mlilo, ndugu, jamaa, marafiki na klabu ya Tanzania Prisons, na kusema
kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini amesema TFF ipo pamoja nao katika
kipindi hichi kigumu cha maombolezo.
Mwili wa marehemu Hassan Mlilo unatarajiwa kusafirishwa leo
mchana kuelekea mkoani Mbeya, ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho
katika mji wa Rujewa mkoani humo.
………………………………………………………………………
Mshambuliaji Mbwana Samatta, juzi Jumatano amerejea katika klabu
yake ya TP Mazembe ya DR Congo, amejikuta katika mazingira mapya baada ya
kukabidhiwa kwa kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Togo, Hubert Velud.
Velud raia wa Ufaransa ambaye pia aliwahi kuwa kocha wa Paris FC
mwaka 1995 mpaka 1999, ambayo kwa sasa inashiriki inashiriki Ligue 2 ya
Ufaransa, ametua Mazembe akitokea Klabu ya USM Alger ya Algeria na kuchukua
mikoba ya Mfaransa mwenzake Patrice Carteron.
Samatta ambaye alikuwa mbioni kutua Genk ya Ubelgiji, dili lake
lilikwama kutokana na mmiliki wa Mazembe, Moise Katumbi kugoma kumuachia.
Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo, ameliambia Championi Ijumaa
kuwa nyota huyo amerejea katika kituo chake cha kazi ili kuweza kuongeza
msukumo wa kuondoka kutokana na Katumbi kutokuwa tayari kupata hasara kutoka
kwa straika huyo.
“Samatta tayari amerejea Congo…Hili litasaidia kumpa presha
Katumbi ya kumuuza maana hatoweza kukubali apate hasara ya jumla, hivyo
atalazimika kukubali matakwa ya mchezaji mwenyewe.
“Lakini pia tumeacha nafasi kwa serikali nayo ione inaweza
kutusaidia vipi kwa kuwasiliana na Katumbi ili kuweza kulimaliza jambo hili,”
alisema Kisongo.
……………………………………………………………..
Baadhi ya mashabiki wa Mbeya City wamemtaka kocha mkuu wa timu
hiyo Meja Mstaafu Abdul Mingange, pamoja na uongozi kuachia ngazi
kutokana na matokeo mabaya ambayo timu hiyo inayapata.
Tangu Mbeya City ilipoanza kuwa chini ya Mingange imeshinda
michezo miwili, imefungwa michezo minne, sare nne.
Kutokana na matokeo hayo mashabiki wengi wamekuwa wakionyesha
kuwa na hasira dhidi ya viongozi.
Wakizungumza na hekaheka viwanajani kwa nyakati tofauti
mashabiki hao walilalama kuwa matokeo hayo yakiendelea hivyo, basi kuna
uwezekano mkubwa wa timu kushuka daraja, hivyo ni bora hatua zikachukuliwa
mapema.
Upande wa uongozi wa Mbeya City kupitia kwa katibu mkuu,
Emmanuel Kimbe, alisema watakaa na benchi la ufundi kujua tatizo na kuwataka
mashabiki kutulia.
…………………………………..
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limejitoa katika sakata la
aliyekuwa nahodha wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ likisema kuwa suala
hilo anahusika nalo kocha mkuu wa timu hiyo, Boniface Mkwasa.
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa alisema suala hilo hawatakiwi
kuliingilia na badala yake wamemuachia kocha mwenyewe.
“Tunashangaa suala hilo kuchukuliwa kubwa na kukuzwa na vyombo
vya habari na mitandao ya kijamii na isitoshe wakati Cannavaro anapewa unahodha
hakupewa barua zaidi ya kuonekana akivaa kitambaa uwanjani.
“Pia maamuzi ya kuichezea au kutoichezea Stars tumemuachia kocha
mwenyewe anayeona mchezaji yupi anafaa kuichezea Stars,” alisema Mwesigwa.
……………………………….
Kweli sasa Yanga hawataki “utani na kazi” baada ya kurejea
kileleni kwa kukausha maji ya mto ruvuma kwa kuitwanga Majimaji ya Songea kwa
mabao 5-0 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Wakati Yanga ikirejea kileleni kwa idadi kubwa ya mabao ya
kufunga na machache ya kufungwa, mshambuliaji wake Amissi Tambwe, amepiga hat
trick.
Tambwe raia wa Burundi amefunga mabao matatu huku mawili
yakifungwa na Wazimbabwe, Donald Ngoma na Thabani Kamusoko aliyefunga la
kwanza.
Kamusoko alifunga bao la kwanza lililodumu hadi mapumziko na
baadaye Yanga ikacharuka kipindi cha pili na kuwatandika vijana wa Kalimangonga
Ongalla aliyewahi kuichezwa Yanga.
Deus Kaseke leo alikuwa mwiba kwa mabeki wa Majimaji
akishirikiana na beki wa kulia, Juma Abdul.
…………………………….
KIMATAIFA..
Liverpool imeamua kumfungia kazi mshambuliaji
wa Shakhtar Donetsk Alex Teixeira kocha Jurgen Klopp akijaribu kufanya usajili
wa kwanza tangu alipotua Anfield. Majogoo hao wa England wako tayari kulipa
pauni milioni 24.5 kwa saini ya mchezaji huyo wa miaka 26. Hata hivyo kilabu
hiyo ya Ukraine inasema kuwa Texeira ambaye pia amehusishwa na uhamisho wa
kwenda Chelsea, atagharimu pauni milioni 39. Klopp anapanga kuimarisha safu
yake ya ushambuliaji huku Danny Ings,Divock Origi na Daniel Sturridge wakiwa
wanauguza majeraha. Wakati Christian Benteke aliyeighrimu kilabu hiyo pauni
milioni 32 akisalia kama mshambuliaji pekee,Liverpool imefunga mabao 25 pekee
katika mechi 22 za ligi msimu huu. Shakhtar ambao wako katika mazoezi mjini
Florida wanamthamini sana Texeira. Amefunga mabao 22 katika mechi 15 na mabao
manne katika mechi 10 za klabu bingwa Ulaya msimu huu. Alianza kuchezea kilabu
ya Vasco da Gama kabla ya kuelekea Shakhtar mwaka 2010.
………………………………………………
Manchester United wamekanusha habari kwamba
walikutana na kuzungumza na meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola kuhusu
uwezekano wake kuwa meneja wao. Hapo kabla tovuti ya France Football ilifichua
hilo na kusema mkutano huo ulifanyika mjini Paris lakini United wamesema habari
hizo si za kweli. Meneja wa sasa wa United Louis van Gaal anakabiliwa na
shinikizo la kutemeshwa kibarua chake baada ya klabu hiyo kutofanya vyema Ligi
Kuu Uingereza na Ulaya. Guardiola tayari ameshaweka wazi kuwa atahamia
Uingereza msimu ujao huku Manchester City na Manchester United zikitajwa
kugombania huduma yake. Guardiola, 45, anataondoka Bayern Munich majira yajayo
ya joto na amesema amepokea maombi kutoka kwa klabu kadha za Uingereza.
………………………………………………
Javier Mascherano amehukumiwa kwenda jela kwa
mwaka mmoja jela pamoja na faini ya pauni 625,000 kwa kukwepa kodi mara mbili.
Hata hivyo mwanasheria wa difenda wa Barcelona na Argentina David Aineto ana
matumaini kuwa mteja wake hatakwenda jela kufuatia jaribio lao la kutaka adhabu
hiyo igeuzwe na kuwa faini. Nyota huyo anadaiwa kutumia ulaghai kukwepa kulipa
kodi ya jumla ya pauni 1.15. Mascherano, 31, awali alikiri makosa mawili ya
kukosa kutangaza mapato yake kamili ya 2011 na 2012. Kwa mujibu wa taratibu za
Hispania, mtu aliyehukumiwa kifungo cha miaka miwili kurudi chini, anaruhusiwa
kulipa faini, labda tu iwe amehukumiwa kwa makosa ya kutumia nguvu au ujangili.
Nyota huyo wa zamani wa Liverpool na West Ham aliandika kwenye Twitter: “Mimi
ni mchezaji soka ya kulipwa, sifahamu sana masuala ya ushuru na sheria.
“Kuangazia masuala hayo magumu, mimi huwategemea watu wengine. “Katika maisha
yangu ya uchezaji, nimekuwa mtu mwaminifu, wa kuwajibika na anayeheshimu
wachezaji wengine na klabu ambazo nimechezea.” Mascherano tayari alishalipa
kiasi kiasi alichokwepa (pauni milioni 1.15) kabla adhabu haijatolewa.
Alihukumiwa kwenda jela kwa miezi minne kwa kosa la kwanza huku kosa la pili
likimpa hukumu ya mieiz minane.
…………………………………..
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uruaguay
anayecheza katika klabu ya Barcelona, Luis Suarez amesema kwamba hatatizwi na
kauli kwamba hakuwa chaguo la kwanza la timu hiyo wakati anasajiliwa. Nyota
huyo aliyehamia kutoka kikosi cha Liverpool amesema kwamba hata kama hakuwa
anatakiwa sana na wenye timu, lakini sasa anajua kwamba wataumiza vichwa tena
wakisikia anataka kuhama. “Sijali kama sikuwa chaguo lao, achana na habari
hiyo. Tuseme sasa nataka kuhama, utasikia habari hiyo kwamba ninatakiwa kuwa wa
kwanza kuuzwa? Najua hakuna anayetamani niondoke leo na hiyo ndio tofauti na
maneno na vitendo,” amesema. Mkurugenzi wa michezo wa zamani wa Barcelona,
Andon Zubizarreta alisema klabu yake iliamua kumsajili Luis Suarez kwa sababu
chaguo lao la kwanza la mchezaji waliyemwitaji hakuwa anauzwa. Ikasemwa kwamba
kauli hii imewashangaza wengi ila ndio ukweli, Luiz Suarez hakuwa chaguo la
kwanza katika usajili wa Barcelona. Suarez mwenyewe amesema kama hakuwa chaguo
sahihi kwa FC Barcelona sasa ndio ametua na anaendelea kufanya vema, watasema
nini tena? Kumbe mshambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero ndio lilikuwa
chaguo la kwanza kwa Barca katika mpango wao wa kupata safu ya ushambuliaji
itakayokuwa na makali kama wapinzani wao, Real Madrid. Zubizarreta juzi
ameeleza kwamba Barca ilimuhitaji Aguero aungane na Lionel Messi na Naymar
kuunda safu ya ushambuliaji itakayoendana na kasi ya BBC ya Real Madrid.
Alisema: “Tulikuwa na machaguo machache, chaguo letu la kwanza halikuwa Suarez,
yeye mwenyewe anajua hili.” “Tulijaribu kumsaini Aguero lakini ikashindikana
na mpaka kufikia hapo hatukuwa na uamuzi mwingine wa kufanya zaidi ya kumsajili
Suarez.” Zubizarreta pia anasema, suala la Suarez kufungiwa kwa kumng’ata beki
wa Italia, Giorgio Chiellini liliwapa nafasi zaidi wao kwa sababu timu nyingine
ziliamua kuachana na mipango yao ya kumtaka mchezaji huyo. Aliongeza: “Wakati
tupo kwenye majadiliano ya Liverpool likatokea lile sakata la Suarez na
Chiellini.” “Suala hili lilileta mashaka makubwa kwenye vichwa vya viongozi wa
timu nyingine waliokuwa wakimtaka Suarez.” “Tabia yake ilikuwa kwenye mjadala
mkubwa na hakuna aliyekuwa anajua atafungiwa kwa muda gani, muda huohuo ndipo
nafasi ya kumsajili ikawa kubwa na tukakamilisha kila kitu.”
……………………………….
NYOTA wa klabu ya Atletico Madrid, Matias
Kranevitter amekiri tetesi za kuwaniwa na timu kadhaa za premier, lakini
Chelsea na Manchester City ndio wanaongoza mbio hizo. Lakini matajiri wa jiji
la London, Chelsea wameongeza kasi ya kumwania kiungo huyo mwenye umri wa miaka
22 kwa ajili ya kutua darajani mwezi huu wa Januari. Awali Kranevitter amekuwa
akihusishwa na tetesi za kutaka kujiunga kwa Washika Mitutu wa jiji la London
na Arsene Wenger ameweka mezani ofa kwa ajili yake. Lakini kocha wa sasa wa
mpito wa matajiri hao, Guus Hiddink inasemekana ameingilia kati dili hilo na
anapambana kuhakikisha kiungo huyo anatua katika kikosi cha Stanford Bridge.
Akinukuliwa, kiungo huyo amesema ndoto zake za kutua Emirates zinaweza kuyeyuka
kwa sababu Hiddink ameongeza kasi ya mazungumzo. “Nimekuwa nikisikia malengo ya
Hiddink kwangu na kadri ninavyotambua mpango uko hivyo.” “Ni kati ya makocha
wazuri duniani wanaovutua kufanya kazi nao, kila mchezaji anaota ndoto ya
kufundishwa na mwalimu wa mfano wake.” “Kwa nyakati tofauti nimekuwa
nikifundishwa na makocha wengine. Kama kuna siku inatokea Napata nafasi ya
kufanya kazi chini yake nitakuwa na furaha kubwa.” “Lakini kwa sasa bado nipo
Atletico. Najisikia furaha kuwa hapa, hakuna tatizo kuwa hapa.” “Kucheza katika
timu inayoshiriki Ligi ya Mabingwa ni kati ya malengo yangu pia. Kila mchezaji
anaota mafanikio kama hayo.” “Ninataraji kuwa katika kiwango hicho cha
mafanikio, ninaamini kuna siku nitafikia hatua hiyo, ni suala la kusubiri
kuona,” alisisitiza Matias Kranevitter.
……………………………………………………..
HABARI zinazomhusu mchezaji wa timu ya taifa
ya Ujerumani, Ilkay Gundogan zinatatanisha. Awali, mwanzoni mwa mwaka huu
imedaiwa kwamba mchezaji huyo hajausaini mkataba wa muda mrefu na Borussia
Dortmund akitaka ahamie katika klabu mpya kwenye Ligi ya Bundesliga. Hata
hivyo, habari mpya ni kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye
amekuwa katika klabu ya Dortmund tangu mwaka 2011, anataka kumfuata kocha wake
aliyekuwa nae kwa muda mrefu, Jurgen Klopp ambaye sasa anakinoa kikosi cha
Liverpool. Gundogan ameliambia gazeti la Bild kuwa hajafanya uamuzi wowote na
lazima atasaini kila kitu kwa sababu urefu ya taaluma ya mtu una ukomo.
Ameongeza kuwa kila kitu kingali wazi na kuwa mkataba wake ujao utakuwa mrefu
na sio wa mwaka mmoja tu. Amesema kwamba anataka kulinda kiwango chake, lakini
haoni kwamba kuna timu ambayo inaweza kusaidia kikosi chake zaidi ya Liverpool
kwa sababu katika kikosi hicho kuna mtu ambaye anajua kwamba anamfaa. Na wala
hafichi, anamtaja mtu huyo kuwa ni Klopp ambaye anadai kuwa alikuwa nae katika
kikosi hicho kwa kiwango cha mtu na kaka yake na alimsaidia sana. “Alikuwa kama
kaka au baba yangu hapa, nikienda Uingereza kwa vyovyote vile sitakwenda
Arsenal au Man United, sitakwenda Chelsea au Man City, nitakwenda Liverpool kwa
sababu ya Klopp,” alisema.
………………………………………………………
ALEX Sandro tayari ameonyesha azma ya kutaka
kuondoka Juventus ili akatafute maisha mbele ya safari katika usajili huu wa
mwezi Januari. Tena amekwenda mbali zaidi kwa kuitaja timu anayoipenda kwenda
kukipiga na kwamba mapenzi yake ni kuvaa uzi wa Manchester City. Mshambuliaji
huyo ameuomba uongozi wa klabu ya Juve licha ya kumruhuasu aondoke, anataka
kwenda kutimiza azma yake ya kucheza Ligi ya premier. Sandro ambaye msimu
huu amekuwa katika kiwango bora akiwa na Juve, ameweka bayana ndoto yake ya
kucheza katika Ligi iliyo na mashabiki wengi. “Nina malengo ya kutimiza ndoto
ya kwenda kucheza katika Ligi ya premier.” “Ninataka kuona ninalinda kipaji
changu, sitaki kuwa msiri juu ya mimi kuondoka hapa.” “Soka ni kazi
ninayokwenda kufanya popote, soka ni mchezo wa kuangalia leo na kesho, huu ndio
msimamo wangu kwa sasa,” alisema Sandro. “Manchester City ni klabu ninayoipenda
kwa ajili ya soka langu la baadae, ninaamini nina nafasi ya kucheza nikiwa kule
na kutimiza ndoto yangu hii,” alisisitiza Sandro raia wa Brazil.
………………………………………………………..
PARIS Saint - Germain sasa ipo tayari kuweka
mezani kitita cha pauni mil. 18 kwa ajili ya kumnasa straika wa Swansea,
Bafetimbi Gomis, hii ni kwa mujibu wa Sky Sports. Straika huyo raia wa Ufaransa
ameingia katika rada za PSG inayotaka kuendeleza ubabe katika Ligi ya Italia.
Dalili za Bafetimbi kutua katika kikosi cha mabingwa watetezi zinatiwa nguvu na
taarifa za kwamba kiwango chake kwa sasa kimewavutia baadhi ya mawakala wa
klabu mbalimbali. Tayari PSG wameteta na wakala wa nyota uyo na kwamba hata
Swansea wenyewe wamethibitisha kuwepo kwa pilika kuhusiana na straika huyo.
Wakitambua hilo, PSG wamemtengea kiungo huyo kitita cha pauni mil. 18
wakiongeza dau waliloliweka awali ambalo lilikuwa pauni mil. 15. PSG walimthaminisha
Mfaransa huyo kuwa ni wad au la mil. 18 ingawa wameonyesha dalili za kukubalim
kushusha kiwango. Swansea pamoja na kuweka bayana thamani ya mchezaji huyo,
wamethibitisha kuwa straika huyo ni miongoni mwa wachezaji wanaotakiwa na klabu
mbalimbali za Ulaya. “Bafetimbi anawindwa na timu nyingi za Ulaya, lakini
nataka acheze katika kikosi ambacho atapambana na kudumu.” “Ni mchezaji mwenye
ofa nyingi, ila ni jambo la kusubiri kuona ifikapo kipindi cha usajili kikifika
mwisho.”
…………………………………………………
STAA wa Arsenal, Mesut Ozil amesema kwamba
hatalazimisha kuongeza mabao zaidi katika timu hiyo na badala yake ataendelea
na kasi yake ya kuwatengenezea wenzake. Kiungo huyo mshambuliaji kwa sasa ni
mmoja kati ya nyota wanaoongoza kuwatengenezea mabao wenzake na kwa sasa ndiye
anayeongoza kufanya kazi hiyo kwenye michuano ya Ligi Kuu England akiwa ametoa
pasi 16. Kwa ujumla Ozil ameshafunga mabao matatu katika mechi 20 alizoichezea
Arsenal msimu huu, lakini Mjerumani huyo anasema kwamba anaona hakuna haja ya kuongeza
idadi hiyo ya mabao yake. “Mwisho wa siku nitajaribu kupata mafanikio kwa kila
mechi ili tuweze kushinda,” staa huyo aliuambia mtandao wa chama cha soka
nchini Ujerumani. “Haijalishi kama nitafunga bao ama nitatoa pasi kwani jambo
la msingi ni kwamba tumeshinda. Sioni kama itakuwa na mana zaidi kama
nitaelekeza nguvu zangu katika kufunga mabao ama kuwa mchoyo nikiwa mbele ya
lango,” aliongeza staa huyo. Ozil alisema kwamba alichokipania ni kuipaisha
Arsenal msimu huu pamoja na timu ya taifa ya Ujerumani katika fainali za
Mataifa ya Ulaya (Euro 2016).
……………………………………………………
MWANASOKA wa zamani, Roberto Carlos amepuuzia
taarifa zinazodai kuwa nyota wa Barcelona, Neymar kwamba anaweza kuhamia kwa
mahasimu wao, Real Madrid. Beki huyo wa zamani wa Real Madrid na timu ya taifa
ya Brazil alisema kwamba anaweza kumhamisha Neymar kutoka Barcelona kwenda Real
Madrid endapo atapewa jukumu la kuinoa klabu hiyo. Jumapili Neymar alikuwa
kwenye ubora wake tena akiwa na Barcelona baada ya kufunga bao moja kati ya
sita ambayo timu yake iliibuka na ushindi huo mnono dhidi ya Athletic Bilbao
katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania, La Liga. Hata hivyo, pamoja na ubora huo
Carlos anapotezea kama kunaweza kukawepo na uwezekano kwa nyota huyo akaitema
Barcelona na kujiunga na Madrid. “Haiwezekani nimewahi kusema hivyo siku za
nyuma na watu wamekuwa wakilichukulia jambo hilo kwa umakini kwa sababu Real
Madrid huwa inasajili wachezaji bora duniani,” alisema Mbrazil huyo ambaye
amerejea katika mji mkuu wa nchi hiyo, Hispania akiwa na timu yake ya zamani
kwa ajili ya maandalizi ya kujiendeleza na kibarua chake cha ukocha. Mshindi
huyo wa Kombe la Dunia alisema kuwa ingekuwa jambo jema kama angeweza kufanya
kazi chini ya kocha mpya wa klabu hiyo, Zinedine Zidane, lakini akasema kuwa dhamira
yake kwa sasa ni kuendelea na mafunzo yake ya ukocha. “Ningefurahi kama
kungekuwepo na uwezekano huo lakini nipo mahali hapa kwa ajili ya mazoezi na
kujifunza,” alisema Carlos na kuongeza kuwa kwa sasa ameanza mafunzo yake ya
ngazi ya juu baada ya kutumia muda wa miaka mitano akifanya hivyo katika nchi
za Uturuki, Urusi na India huku akisema ameshajifunza mengi lakini anaomba
apewe muda.
………………………………………………………………
STRAIKA wa timu ya Feyenoord, Colin
Kazim-Richards amemtetea staa wa Man Utd, Mephis Depay akisema kwamba shutuma
zinazomkabili ndizo zitakazomfanya ang’are. Depay aling’ara wakati wa fainali
za Kombe la Dunia za mwaka 2014 baada ya kuiwezesha Uholanzi ushika nafasi ya
13 na huku msimu huu akiibuka mfungaji bora katika Ligi ya Eredevisie akiwa na
mabao 22 yaliyoipa ubingwa PSV msimu wa 2014/15. Kiwango hicho ndicho
kilichomfanya asajiliwe kwa bei kubwa na Man United, lakini tangu atue kwenye
klabu hiyo, staa huyo mwenye umri wa miaka 21 ameshindwa kung’ara na hivyo
kuandamwa na shutuma. Hata hivyo, Kazim-Richards ambaye juzi alitemwa kwenye
kikosi cha kwanza cha Feyenoord, ambacho juzi kilikuwa kikiivaa PSV bada ya
kuwaponda waandishi, anaamini kwamba shutuma hizo ndizo zitakazomjenga staa
huyo.
…………………………………………………………..
LIGI
KUU YA HISPANIA KUENDELEA TENA WEEKEND HII KWA MECHI KADHAAAAA/
LEO Jumamosi
Malaga v Barcelona
Saa 12:00 Jioni
Espanyol Villarreal
Saa 2:15 Usiku
Granada v Getafe
Saa 4:30 Usiku
KESHO Jumapili
Athletic v Eibar
Saa 8:00 Mchana
Atletico v Sevilla
Saa 12:00 Jioni
Deportivo v Valencia
Saa 2:15 Usiku
Betis v Real Madrid
Saa 4:30 Usiku.
Friends Rangers timu ya Ligi Daraja la Kwanza, imepanga kuwatumia mastraika wake hatari ambao wamewahi kucheza katika klabu za Sweden na Dubai ili kuhakikisha wanashinda mechi hiyo.
Ofisa habari wa klabu hiyo Asha Kigundula, amesema licha ya kujua wanacheza na timu inayoongoza Ligi Kuu, wao wamejipanga kushinda mchezo huo.
"Kikosi chetu kipo kambini na kila kitu kinakwenda vizuri kabisa kwa ajili ya kujiandaa na mechi hiyo ya Jumapili.
"Tumejipanga kushinda hivyo Yanga ifute ndoto za kutufunga kwa sababu juzi ilipata ushindi wa mabao mengi, wameifunga timu ambayo ilipanda kizengwe wasubili waone tutakachowafanya"alisema Kigundula
Hata hivyo Kigundula amewataka mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi katika mchezo wao ili waweze kuwapa hali zaidi wachezaji wao wacheze kwa kujiamini.
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa alisema suala hilo hawatakiwi kuliingilia na badala yake wamemuachia kocha mwenyewe.
………………………………………………
………………………………………………
…………………………………..
……………………………….
……………………………………………………..
………………………………………………………
………………………………………………………..
…………………………………………………
……………………………………………………
………………………………………………………………
…………………………………………………………..
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
Atletico
de Madrid
|
20
|
15
|
2
|
3
|
30
|
8
|
22
|
47
|
2
|
Barcelona
|
19
|
14
|
3
|
2
|
50
|
15
|
35
|
45
|
3
|
Real
Madrid
|
20
|
13
|
4
|
3
|
57
|
19
|
38
|
43
|
4
|
Villarreal
|
20
|
12
|
4
|
4
|
26
|
16
|
10
|
40
|
5
|
Celta
de Vigo
|
20
|
10
|
4
|
6
|
32
|
30
|
2
|
34
|
6
|
Eibar
|
20
|
9
|
6
|
5
|
32
|
21
|
11
|
33
|
7
|
Sevilla
|
20
|
9
|
5
|
6
|
28
|
22
|
6
|
32
|
8
|
Deportivo
de La Coruna
|
20
|
6
|
10
|
4
|
27
|
24
|
3
|
28
|
9
|
Athletic
Club
|
20
|
8
|
4
|
8
|
27
|
28
|
-1
|
28
|
10
|
Getafe
|
20
|
7
|
5
|
8
|
24
|
28
|
-4
|
26
|
11
|
Valencia
CF
|
20
|
5
|
9
|
6
|
25
|
21
|
4
|
24
|
12
|
Malaga
|
20
|
6
|
6
|
8
|
15
|
17
|
-2
|
24
|
13
|
Real
Sociedad
|
21
|
5
|
6
|
10
|
24
|
33
|
-9
|
21
|
14
|
Espanyol
|
20
|
6
|
3
|
11
|
18
|
33
|
-15
|
21
|
15
|
Real
Betis
|
20
|
5
|
6
|
9
|
13
|
28
|
-15
|
21
|
16
|
Las
Palmas
|
20
|
4
|
6
|
10
|
19
|
30
|
-11
|
18
|
17
|
Sporting
de Gijon
|
20
|
5
|
3
|
12
|
22
|
35
|
-13
|
18
|
18
|
Granada
CF
|
20
|
4
|
5
|
11
|
21
|
41
|
-20
|
17
|
19
|
Rayo
Vallecano
|
20
|
4
|
4
|
12
|
23
|
45
|
-22
|
16
|
20
|
Levante
|
20
|
3
|
5
|
12
|
17
|
36
|
-19
|
14
|
………………………………………………………………..
LIGI
KUU ENGLAND KUENDELEA WEEKEND HII
English
Barclays Premier League
|
||||
14:45
|
Norwich
City
|
v
|
Liverpool
|
Carrow
Road
|
17:00
|
Crystal
Palace
|
v
|
Tottenham
Hotspur
|
Selhurst
Park
|
17:00
|
Leicester
City
|
v
|
Stoke
City
|
King
Power Stadium
|
17:00
|
Manchester
United
|
v
|
Southampton
|
Old
Trafford
|
17:00
|
Sunderland
|
v
|
Bournemouth
|
Stadium
of Light
|
17:00
|
Watford
|
v
|
Newcastle
United
|
Vicarage
Road
|
17:00
|
West
Bromwich Albion
|
v
|
Aston
Villa
|
The
Hawthorns
|
19:30
|
West
Ham United
|
v
|
Manchester
City
|
Boleyn
Ground
|
English
Football League Championship
|
||||
14:30
|
Queens
Park Rangers
|
v
|
Wolverhampton
Wanderers
|
Loftus
Road Stadium
|
17:00
|
Birmingham
City
|
v
|
Ipswich
Town
|
St.
Andrew's Stadium
|
17:00
|
Bolton
Wanderers
|
v
|
MK
Dons
|
Macron
Stadium
|
17:00
|
Brighton
and Hove Albion
|
v
|
Huddersfield
Town
|
Amex
Stadium
|
17:00
|
Cardiff
City
|
v
|
Rotherham
United
|
Cardiff
City Stadium
|
17:00
|
Charlton
Athletic
|
v
|
Blackburn
Rovers
|
The
Valley
|
17:00
|
Fulham
|
v
|
Hull
City
|
Craven
Cottage
|
17:00
|
Leeds
United
|
v
|
Bristol
City
|
Elland
Road
|
17:00
|
Middlesbrough
|
v
|
Nottingham
Forest
|
Riverside
Stadium
|
17:00
|
Preston
North End
|
v
|
Brentford
|
Deepdale
|
17:00
|
Reading
|
v
|
Sheffield
Wednesday
|
Madejski
Stadium
|
French
Ligue 1
|
||||
18:00
|
Paris
Saint-Germain
|
v
|
Angers
|
Parc
des Princes
|
21:00
|
Guingamp
|
v
|
Bastia
|
Stade
Municipal de Roudourou
|
21:00
|
Lille
|
v
|
Troyes
|
Stade
Pierre-Mauroy
|
21:00
|
Montpellier
|
v
|
Caen
|
Stade
de la Mosson
|
21:00
|
Nantes
|
v
|
Bordeaux
|
La
Beaujoire-Louis-Fonteneau
|
21:00
|
Nice
|
v
|
Lorient
|
Allianz
Riviera
|
German
Bundesliga
|
||||
16:30
|
1.
FC Koln
|
v
|
VfB
Stuttgart
|
RheinEnergieStadion
|
16:30
|
FC
Ingolstadt 04
|
v
|
1.
FSV Mainz 05
|
Audi
Sportpark
|
16:30
|
Hannover
96
|
v
|
SV
Darmstadt 98
|
HDI-Arena
|
16:30
|
Hertha
BSC
|
v
|
FC
Augsburg
|
Olympiastadion
|
16:30
|
TSG
1899 Hoffenheim
|
v
|
Bayer
04 Leverkusen
|
WIRSOL
Rhein-Neckar-Arena
|
19:30
|
Borussia
Monchengladbach
|
v
|
Borussia
Dortmund
|
Borussia-Park
|
Italian
Serie A
|
||||
19:00
|
Frosinone
|
v
|
Atalanta
|
Matusa
|
21:45
|
Empoli
|
v
|
Milan
|
Carlo
Castellani
|
MultiChoice
Diski Challenge
|
||||
10:00
|
Bloemfontein
Celtic
|
v
|
Platinum
Stars
|
Siwelele
Park
|
10:00
|
Kaizer
Chiefs
|
v
|
Black
Aces
|
Dobsonville
Stadium
|
10:00
|
SuperSport
United
|
v
|
Bidvest
Wits
|
Bidvest
Stadium
|
National
First Division
|
||||
15:30
|
Moroka
Swallows
|
v
|
AmaZulu
|
Dobsonville
Stadium
|
15:30
|
Witbank
Spurs
|
v
|
Santos
|
Puma
Rugby Stadium
|
15:30
|
FC
Cape Town
|
v
|
Black
Leopards
|
NNK
Rugby Stadium
|
15:30
|
Thanda
Royal Zulu FC
|
v
|
Vasco
Da Gama
|
Umhlathuze
Sports Complex
|
15:30
|
Baroka
FC
|
v
|
Mthatha
Bucks
|
Old
Peter Mokaba Stadium
|
Portuguese
Primeira Liga
|
||||
18:00
|
Moreirense
|
v
|
Estoril
Praia
|
Parque
Joaquim de Almeida Freitas
|
18:00
|
União
da Madeira
|
v
|
CD
Nacional
|
Estádio
do Centro Desportivo da Madeira
|
20:30
|
Benfica
|
v
|
Arouca
|
Estadio
da Luz
|
22:45
|
Paços
de Ferreira
|
v
|
Sporting
Lisbon
|
Estádio
Mata Real
|
Rwanda
2016 Chan
|
||||
15:00
|
Zimbabwe
|
v
|
Mali
|
Rubavu
|
Spanish
La Liga
|
||||
17:00
|
Malaga
|
v
|
Barcelona
|
La
Rosaleda
|
19:15
|
Espanyol
|
v
|
Villarreal
|
RCDE
Stadium
|
21:30
|
Granada
CF
|
v
|
Getafe
|
Los
Carmenes
|
23:05
|
Rayo
Vallecano
|
v
|
Celta
de Vigo
|
Campo
de Futbol de Vallecas
|
24 January 2016
|
||||
Absa
Premiership
|
||||
15:30
|
Kaizer
Chiefs
|
v
|
Platinum
Stars
|
Cape
Town Stadium
|
15:30
|
University
of Pretoria
|
v
|
Black
Aces
|
Loftus
Versfeld Stadium
|
15:30
|
Chippa
United
|
v
|
Ajax
Cape Town
|
Buffalo
City Stadium
|
English
Barclays Premier League
|
||||
15:30
|
Everton
|
v
|
Swansea
City
|
Goodison
Park
|
18:00
|
Arsenal
|
v
|
Chelsea
|
Emirates
Stadium
|
French
Ligue 1
|
||||
15:00
|
Monaco
|
v
|
Toulouse
|
Stade
Louis II
|
18:00
|
Reims
|
v
|
St
Etienne
|
Stade
Auguste-Delaune
|
22:00
|
Lyon
|
v
|
Marseille
|
Stade
des Lumieres
|
German
Bundesliga
|
||||
16:30
|
Eintracht
Frankfurt
|
v
|
VfL
Wolfsburg
|
Commerzbank
Arena
|
18:30
|
FC
Schalke 04
|
v
|
SV
Werder Bremen
|
VELTINS-Arena
|
Italian
Serie A
|
||||
13:30
|
Fiorentina
|
v
|
Torino
|
Artemio
Franchi
|
16:00
|
Internazionale
|
v
|
Carpi
|
Giuseppe
Meazza
|
16:00
|
Lazio
|
v
|
Chievo
|
Olimpico
|
16:00
|
Palermo
|
v
|
Udinese
|
Renzo
Barbera
|
16:00
|
Sampdoria
|
v
|
Napoli
|
Luigi
Ferraris
|
16:00
|
Sassuolo
|
v
|
Bologna
|
Città
del Tricolore
|
16:00
|
Verona
|
v
|
Genoa
|
Marc'Antonio
Bentegodi
|
21:45
|
Juventus
|
v
|
Roma
|
Juventus
Stadium
|
MultiChoice
Diski Challenge
|
||||
10:00
|
Chippa
United
|
v
|
Golden
Arrows
|
Wolfson
Stadium
|
10:00
|
University
of Pretoria
|
v
|
Polokwane
City
|
Loftus
Stadium
|
12:00
|
Free
State Stars
|
v
|
Orlando
Pirates
|
Clarens
Stadium
|
12:00
|
Jomo
Cosmos
|
v
|
Mamelodi
Sundowns
|
Olen
Park Stadium
|
National
First Division
|
||||
15:30
|
African
Warriors
|
v
|
Highlands
Park
|
Charles
Mopeli Stadium
|
15:30
|
Royal
Eagles
|
v
|
Mbombela
United
|
King
Zwelithini Stadium
|
Portuguese
Primeira Liga
|
||||
18:00
|
Belenenses
|
v
|
Vitória
Guimarães
|
Estadio
do Restelo
|
20:15
|
Sporting
Braga
|
v
|
Rio
Ave
|
Estadio
Municipal de Braga
|
22:30
|
FC Porto
|
v
|
Marítimo
|
Estadio
do Dragao
|
Rwanda
2016 Chan
|
||||
16:00
|
Morocco
|
v
|
Rwanda
|
Amahoro,
Kigali
|
16:00
|
Ivory
Coast
|
v
|
Gabon
|
Stade
Huye
|
Spanish
La Liga
|
||||
13:00
|
Athletic
Club
|
v
|
Eibar
|
San
Mames
|
17:00
|
Atletico
de Madrid
|
v
|
Sevilla
|
Vicente
Calderon
|
19:15
|
Deportivo
de La Coruna
|
v
|
Valencia
CF
|
Riazor
|
21:30
|
Real
Betis
|
v
|
Real
Madrid
|
Benito
Villamarin
|
……………………………………………………………..
MSIMAMO
WA LIGI MBALI MBALI.
English Barclays Premier League |
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
Arsenal
|
22
|
13
|
5
|
4
|
37
|
21
|
16
|
44
|
2
|
Leicester
City
|
22
|
12
|
8
|
2
|
39
|
26
|
13
|
44
|
3
|
Manchester
City
|
22
|
13
|
4
|
5
|
43
|
21
|
22
|
43
|
4
|
Tottenham
Hotspur
|
22
|
10
|
9
|
3
|
38
|
18
|
20
|
39
|
5
|
Manchester
United
|
22
|
10
|
7
|
5
|
28
|
20
|
8
|
37
|
6
|
West
Ham United
|
22
|
9
|
8
|
5
|
34
|
26
|
8
|
35
|
7
|
Stoke
City
|
22
|
9
|
6
|
7
|
24
|
22
|
2
|
33
|
8
|
Crystal
Palace
|
22
|
9
|
4
|
9
|
23
|
24
|
-1
|
31
|
9
|
Liverpool
|
22
|
8
|
7
|
7
|
25
|
28
|
-3
|
31
|
10
|
Southampton
|
22
|
8
|
6
|
8
|
31
|
24
|
7
|
30
|
11
|
Everton
|
22
|
6
|
11
|
5
|
39
|
32
|
7
|
29
|
12
|
Watford
|
22
|
8
|
5
|
9
|
25
|
25
|
0
|
29
|
13
|
West
Bromwich Albion
|
22
|
7
|
6
|
9
|
22
|
30
|
-8
|
27
|
14
|
Chelsea
|
22
|
6
|
7
|
9
|
31
|
34
|
-3
|
25
|
15
|
Bournemouth
|
22
|
6
|
6
|
10
|
26
|
37
|
-11
|
24
|
16
|
Norwich
City
|
22
|
6
|
5
|
11
|
24
|
38
|
-14
|
23
|
17
|
Swansea
City
|
22
|
5
|
7
|
10
|
20
|
30
|
-10
|
22
|
18
|
Newcastle
United
|
22
|
5
|
6
|
11
|
24
|
39
|
-15
|
21
|
19
|
Sunderland
|
22
|
5
|
3
|
14
|
27
|
45
|
-18
|
18
|
20
|
Aston
Villa
|
22
|
2
|
6
|
14
|
18
|
38
|
-20
|
12
|
……………………………………………………………………….
German Bundesliga |
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
FC
Bayern Munchen
|
18
|
16
|
1
|
1
|
48
|
9
|
39
|
49
|
2
|
Borussia
Dortmund
|
17
|
12
|
2
|
3
|
47
|
23
|
24
|
38
|
3
|
Hertha
BSC
|
17
|
10
|
2
|
5
|
26
|
18
|
8
|
32
|
4
|
Borussia
Monchengladbach
|
17
|
9
|
2
|
6
|
34
|
30
|
4
|
29
|
5
|
Bayer
04 Leverkusen
|
17
|
8
|
3
|
6
|
25
|
20
|
5
|
27
|
6
|
FC
Schalke 04
|
17
|
8
|
3
|
6
|
23
|
23
|
0
|
27
|
7
|
VfL
Wolfsburg
|
17
|
7
|
5
|
5
|
26
|
21
|
5
|
26
|
8
|
1.
FSV Mainz 05
|
17
|
7
|
3
|
7
|
23
|
23
|
0
|
24
|
9
|
1.
FC Koln
|
17
|
6
|
6
|
5
|
18
|
21
|
-3
|
24
|
10
|
Hamburger
SV
|
18
|
6
|
4
|
8
|
20
|
25
|
-5
|
22
|
11
|
FC
Ingolstadt 04
|
17
|
5
|
5
|
7
|
11
|
18
|
-7
|
20
|
12
|
FC
Augsburg
|
17
|
5
|
4
|
8
|
21
|
26
|
-5
|
19
|
13
|
SV
Darmstadt 98
|
17
|
4
|
6
|
7
|
17
|
26
|
-9
|
18
|
14
|
Eintracht
Frankfurt
|
17
|
4
|
5
|
8
|
21
|
28
|
-7
|
17
|
15
|
VfB
Stuttgart
|
17
|
4
|
3
|
10
|
22
|
37
|
-15
|
15
|
16
|
SV
Werder Bremen
|
17
|
4
|
3
|
10
|
17
|
32
|
-15
|
15
|
17
|
Hannover
96
|
17
|
4
|
2
|
11
|
18
|
29
|
-11
|
14
|
18
|
TSG
1899 Hoffenheim
|
17
|
2
|
7
|
8
|
17
|
25
|
-8
|
13
|
……………………………………………….
Italian Serie A | LOGS
Pos
|
Team
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
1
|
Napoli
|
20
|
13
|
5
|
2
|
41
|
16
|
25
|
44
|
2
|
Juventus
|
20
|
13
|
3
|
4
|
37
|
15
|
22
|
42
|
3
|
Internazionale
|
20
|
12
|
4
|
4
|
25
|
13
|
12
|
40
|
4
|
Fiorentina
|
20
|
12
|
2
|
6
|
37
|
21
|
16
|
38
|
5
|
Roma
|
20
|
9
|
8
|
3
|
37
|
23
|
14
|
35
|
6
|
Milan
|
20
|
9
|
5
|
6
|
27
|
23
|
4
|
32
|
7
|
Sassuolo
|
20
|
8
|
8
|
4
|
25
|
21
|
4
|
32
|
8
|
Empoli
|
20
|
9
|
4
|
7
|
25
|
24
|
1
|
31
|
9
|
Lazio
|
20
|
8
|
4
|
8
|
25
|
29
|
-4
|
28
|
10
|
Chievo
|
20
|
7
|
6
|
7
|
26
|
22
|
4
|
27
|
11
|
Torino
|
20
|
7
|
5
|
8
|
27
|
26
|
1
|
26
|
12
|
Atalanta
|
20
|
7
|
4
|
9
|
21
|
24
|
-3
|
25
|
13
|
Udinese
|
20
|
7
|
3
|
10
|
18
|
31
|
-13
|
24
|
14
|
Sampdoria
|
20
|
6
|
5
|
9
|
29
|
32
|
-3
|
23
|
15
|
Bologna
|
20
|
7
|
2
|
11
|
22
|
27
|
-5
|
23
|
16
|
Genoa
|
20
|
6
|
4
|
10
|
23
|
26
|
-3
|
22
|
17
|
Palermo
|
20
|
6
|
3
|
11
|
19
|
33
|
-14
|
21
|
18
|
Carpi
|
20
|
4
|
5
|
11
|
19
|
35
|
-16
|
17
|
19
|
Frosinone
|
20
|
4
|
3
|
13
|
22
|
45
|
-23
|
15
|
20
|
Verona
|
20
|
0
|
9
|
11
|
13
|
32
|
-19
|
9
|
MWISHOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO.