Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

KIBO FM ADHUHURI YA REDIO KIBO FM. 96.5Mhz.

Views:
Video Information

KIBO FM ADHUHURI.                                10/12/2015.

MIMI..............

 

Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete amesema katika uongozi wake wa miaka 10, hakuwahi kuagiza mtu asamehewe kontena lake lisilipe kodi na angefanya hivyo, mapato ya Serikali yasingeongezeka kutoka Sh bilioni 177 kwa mwezi mpaka Sh bilioni 900.

Akizungumza baada ya kuwashitukiza wananchi wa Chalinze katika soko kuu la eneo hilo kwa kuungana nao kufanya usafi kuitikia agizo la Rais John Magufuli jana asubuhi, Kikwete alisema katika uongozi wake hakuwahi kuagiza mtu anayestahili kulipa kodi asilipe kodi.

Amesema wakati huu ambao amepumzika baada ya kustaafu, amepata nafasi ya kusoma mitandao na magazeti mbalimbali na kukuta baadhi ya watu, wakimshutumu na kumtukana yeye na familia yake wakimhusisha na ukwepaji kodi.

Kikwete amewataka Watanzania wamuunge mkono Rais Magufuli katika jitihada anazofanya za kukabiliana na wakwepa kodi, huku akitoa mfano akisema wakwepa kodi kwa Serikali ni kama inzi na kidonda, hawaondoki bila kufukuzwa na ukiacha kuwafukuza wanarudi.

Pia amesema uamuzi wa Rais Magufuli wa kutumia maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru, kuwataka wananchi wote wafanye usafi, ni wa busara na si wa kukurupuka kwa kuwa mwaka huu taifa lilikabiliwa na ugonjwa wa kipindupindu.

.................................................

Wamiliki na mawakala wa usafiri wa mabasi yaendayo mikoani wameonywa kutopandisha nauli katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria, ikiwamo kufungwa jela.

Onyo hilo limetolewa na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mohammed Mpinga wakati wa uzinduzi wa huduma mpya kwa abiria wa bodaboda kwa njia ya simu ya ‘Fasta Fasta Service’ ambayo itamwezesha abiria kupata huduma hiyo kwa kufuatwa mahali alipo.

Kamanda Mpinga amesema imekuwa ni tabia ya wamiliki wa usafiri wa mabasi hayo pamoja na mawakala wao kuongeza nauli hizo kinyume cha sheria na taratibu zilizowekwa jambo ambalo linawaumiza wananchi.

Amesema Polisi Kikosi cha Barabarani kimejipanga nchi nzima ili kuhakikisha wanakomesha vitendo hivyo na si tu kwa Kituo cha Ubungo pia kwa kupandikiza abiria watakaokuwa na kazi ya kutoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa wahusika.

..................................................

Rais wa Argentina aliyemaliza muda wake , Cristina Fernandez de Kirchner, amewaaga maelfu ya wafuasi wake ambao walikusanyika katikati mwa mji wa Buenos Aires.

Katika hotuba yake ambayo ilijaa hisia nje ya ikulu, Fernandez alivishutumu vyombo vya habari vya nchi hiyo kwa kuipiga vita serikali yake ya mrengo wa kushoto.

Fernandez na mume wake ambae tayari ameaga dunia, Nestor Kirchner, wamekuwa madarakani kwa muda wa miaka kumi na mbili.

Ametetea hali ya uchumi, na kusema hakuna katika utawala uliopita ambao uliiacha Argentina bila madeni.

Na kuwataka raia wa Argentia kutetea haki zao na maslahi yao ambayo wameyapata.

Makundi yaliyokusanyika katika eneo hilo yalikuwa yakiimba wakati Fernandezi akipanda katika jukwaa.

................................................

Mwanaharakati wa haki za binadamu Leyla Yunus ameachiliwa huru Jumatano wiki hii na vyombo vya sheria vya Azerbaijani kwa sababu za kiafya baada zaidi ya mwaka mmoja akiwa jela, huku nchi nyingi za magharibi na mashirika yasio ya kiserikali wakitoa wito wa kuachiliwa kwake.

Mahakama ya Rufaa ya Baku imepunguza hukumu ya miaka minane na nusu jela dhidi ya Leyla Yunus hadi miaka mitano, ikitetea uamuzi wake kwamba hali ya afya ya mwanaharakati huyo, ambaye anasumbuliwa na ini na ugonjwa wa kisukari, imeendelea kuzorota.

Bi Yunus, mwenye umri wa miaka 59, alikamatwa na kuwekwa rumandekwa muda akiwa na mumewe Arif katika majira ya joto 2014 kwa kosa la usaliti na ukwepaji wa kodi, tuhuma ambazo wanandoa hao wamekanusha.

Mwisho wa kibo fm adhuhuri,jiunge nasi tena ifikapo saa kumi kamili kusikiliza kibo fm alasiri.

 

 

 
Similar Videos