Video Information

Makabiliano yameanza upya leo kati ya waandamanaji na polisi mjini Kiev
Watu wawili wameripotiwa kuuwawa
katika mji mkuu wa Ukraine Kiev katika makabiliano yaliyozuka upya kati
ya polisi na waandamanaji wakati polisi walipovamia vizuizi
vilivyowekwa na waandamanaji hao.
Waandamanaji hao walirusha mabomu ya petroli
pamoja na mawe huku polisi wakijibu kwa kuwafyatulia risasi za mpira,
maguruneti ya kuwaduwaza na gesi ya kutoa machozi.Kumeripotiwa ghasia chache usiku kucha mjini Kiev, baada ya vurugu kumalizika.
Vijana walikabiliana kwa mbali na polisi wa kupambana na ghasia walioshika doria nje ya majengo ya bunge. Wiki jana bunge la Ukraine lilipitisha sheria mpya kupiga marufuku maandamano ya hivi karibuni nchini humo.
Sheria hio imeweka kifungo cha miaka mitano kwa wote watakaopatikana wakizingira majengo ya bunge.
Pia ni hatia kuweka kizuizi bila kibali.Waziri Mkuu wa Ukraine Mykola Azarov ameonya kutumia nguvu ikiwa maandamano nchini mwake yataendelea.
Tayari mamia ya polisi na waandamanaji wamejeruhiwa kwenye makabiliano hayo. Baadhi ya waandamaji walipoteza macho baada ya kupigwa risasi za mpira.