Video Information

Hii ni mara ya kwanza kwa Everton kuifunga Man United Uwanjani Old Trafford tangu Mwaka 1992 na kipigo hicho kimewaacha Man United wawe Nafasi ya 9 Pointi 12 nyuma ya Vianara Arsenal.
Bao la ushindi la Everton lilifungwa na Bryan Oviedo katika Dakika ya 86 na kuipa Everton ushindi wa Bao 1-0 ikiwa ni Mechi ya kwanza kwa Meneja wa Man United David Moyes kuivaa Timu yake ya zamani Everton.
Vinara wa Ligi Arsenal waliichapa Hull Cuty Bao 2-0 kwa Bao za Nicklas Bendtner na Mesut Ozil na kuwaweka Pointi 4 juu kileleni mwa Ligi.
Katika Mechi za Jana, shujaa ni Luis Suarez aliepachika Bao 4 wakati Liverpool inaichapa Norwich City Bao 5-1 na kuweka Historia ya kuwa Mchezaji wa kwanza katika Ligi Kuu England kufunga Hetitriki 3 dhidi ya Klabu hiyo hiyo moja.
Katika Misimu miwili iliyopita, Suarez amekuwa akipiga Hetitriki Uwanjani Carrow Road Nyumabini kwa Norwich City.
Bao jingine la 5 la Liverpool lilifungwa na Raheem Sterling.
Huko Stadium of Light, ilikuwa piga nikupige kati ya Sunderland na Chelsea hadi Chelsea kuibuka Mshindi kwa Bao 4-3.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Eden Hazard (Dakika ya 36 na 62 minutes), Frank Lampard (17) na Bao la kujifungwa mwenyewe Phil Bardsley (84) huku Sunderland wakifunga toka kwa Jozy Altidore (14), John O'Shea (50) na Bardsley (86).
Manchester City nao walikuwa na mshikemshike na West Brom na hatimae kushinda Bao 3-2 na kujiweka Pointi 2 nyuma ya Chelsea na Pointi 1 mbele ya Liverpool na Everton.
Bao za Man City zilifungwa na Yaya Toure, Bao 2, na Sergio Aguero na kujikuta wakiongoza lakini WBA wakaja juu na kupiga Bao 2 kupitia Costel Pantilimon, aliejifunga mwenyewe na Victor Anichebe.
LIGI KUU ENGLAND
MATOKEO:
Jumatano Desemba 4
Arsenal 2 Hull City 0
Liverpool 5 Norwich 1
Man United 0 Everton 1
Southampton 2 Aston Villa 3
Stoke 0 Cardiff 0
Sunderland 3 Chelsea 4
Swansea 3 Newcastle 0
Fulham 1 Tottenham 2
West Brom 2 Man City 3
LIVERPOOL 5 NORWICH 1
VIKOSI:
Liverpool: Mignolet, Johnson, Flanagan, Agger, Skrtel, Allen, Gerrard, Henderson, Sterling, Coutinho, Suarez
Norwich: Ruddy; Martin, R Bennett, Bassong, Olsson; Johnson, Fer, Howson, Hoolahan, Redmond, Elmander.
SUNDERLAND 3 CHELSEA 4
VIKOSI:
Sunderland: Mannone, Bardsley, Brown, O'Shea, Dossena, Ki, Giaccherini, Gardner, Colback, Borini, Altidore
Akiba: Larsson, Fletcher, Johnson, Celustka, Pickford, Roberge, Cattermole.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Ramires, Lampard, Willian, Mata, Hazard, Torres
Akiba: Cole, Essien, Mikel, Schurrle, De Bruyne, Ba, Schwarzer.
Refa: Phil Dowd
STOKE 0 CARDIFF 0
VIKOSI:
Stoke: Begovic, Cameron, Shawcross, Wilson, Pieters, Nzonzi, Whelan, Arnautovic, Adam, Assaidi, Crouch
Akiba: Muniesa, Pennant, Palacios, Jones, Walters, Sorensen, Ireland.
Cardiff: Marshall, Theophile-Catherine, Caulker, Turner, John, Medel, Cowie, Gunnarsson, Mutch, Whittingham, Campbell
Akiba: Connolly, Hudson, Cornelius, Odemwingie, Kim, Noone, Lewis.
Refa: Michael Oliver
MAN UNITED 0 EVERTON 1
VIKOSI:
Manchester United: De Gea; Rafael, Vidic, Smalling, Evra; Valencia, Fellaini, Giggs, Kagawa, Welbeck; Rooney.
Everton: Howard, Oviedo, Distin, Jagielka, Coleman, McCarthy, Barry, Pienaar, Barkley, Mirallas, Lukaku
ARSENAL 2 HULL CITY 0
VIKOSI:
Arsenal: Szczesny, Jenkinson, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Flamini, Ramsey, Rosicky, Cazorla, Ozil, Bendtner
Hull: McGregor, Figueroa, Elmohamady, Chester, Bruce, Meyler, Huddlestone, Livermore, Brady, Graham, Sagbo
SWANSEA 3 NEWCASTLE 0
VIKOSI:
Swansea: Vorm, Tiendalli, Chico, Williams, Ben Davies, Canas, de Guzman, Pozuelo, Shelvey, Hernandez, Vazquez
Akiba: Amat, Taylor, Britton, Dyer, Lamah, Routledge, Tremmel.
Newcastle: Krul, Debuchy, Williamson, Coloccini, Santon, Sissoko, Tiote, Cabaye, Gouffran, Remy, Shola Ameobi
Akiba: Anita, Dummett, Yanga-Mbiwa, Haidara, Elliot, Obertan, Sammy Ameobi.
Refa: Howard Webb
SOUTHAMPTON 2 ASTON VILLA 3
VIKOSI:.
Southampton: Gazzaniga, Clyne, Yoshida, Lovren, Shaw, Wanyama, S. Davis, Ward-Prowse, Lallana, Rodriguez, Lambert
Aston Villa: Guzan, Bacuna, Vlaar, Clark, Baker, Luna, El Ahmadi, Westwood, Delph, Agbonlahor, Kozak
FULHAM 1 TOTTENHAM 2
Fulham: Stekelenburg, Riether, Hughes, Senderos, Riise, Karagounis, Parker, Kasami, Dejagah, Kacaniklic, Berbatov
Akiba: Sidwell, Ruiz, Stockdale, Duff, Taarabt, Zverotic, Boateng.
Spurs: Lloris, Walker, Chiriches, Dawson, Vertonghen, Capoue, Sandro, Lennon, Paulinho, Lamela, Defoe
Akiba: Soldado, Holtby, Naughton, Townsend, Chadli, Sigurdsson, Friedel.
Refa: Mark Clattenburg
WEST BROM 2 MAN CITY 3
West Brom: Myhill, Reid, McAuley, Olsson, Ridgewell, Morrison, Yacob, Amalfitano, Berahino, Brunt, Long
Akiba: Popov, Lugano, Anichebe, Daniels, Vydra, Gera, Sessegnon.
Man City: Pantilimon, Zabaleta, Demichelis, Kompany, Kolarov, Jesus Navas, Fernandinho, Toure, Nasri, Dzeko, Aguero
Akiba: Hart, Richards, Lescott, Milner, Negredo, Javi Garcia, Rodwell.
Refa: Chris Foy
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Desemba 7
1545 Man United v Newcastle
1800 Crystal Palace v Cardiff
1800 Liverpool v West Ham
1800 Southampton v Man City
1800 Stoke v Chelsea
1800 West Brom v Norwich
2030 Sunderland v Tottenham
Jumapili Desemba 8
1630 Fulham v Aston Villa
1900 Arsenal v Everton
Jumatatu Desemba 9
2300 Swansea v Hull