Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

KOMBE LA DUNIA-AFRIKA: SAFARI YA BRAZIL KUANZA JUMAMOSI!!

Views:
Video Information

BRAZIL_2014_BESTMASTAA wa AFRIKA, kina Didier Drogba, Samuel Eto'o, Asamoah Gyan, John Obi Mikel na Jonathan Pitroipa, Wikiendi hii wataongoza Nchi zao kusaka Tiketi ya kwenda Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia Mwakani wakati Mechi za Raundi ya Mwisho ya Mtoano ztakapochezwa.
Zipo Nchi 10 ambazo zimepangiwa Mechi 5, za Nyumbani na Ugenini, na Washindi watano ndio watakaoenda Brazil.
Ivory Coast watamtegemea Didier Drogba watakapocheza na Senegal kwenye Mechi ya kwanza Mjini Abidjan huku Cameroun wakifurahia kwa Straika wao hatari Samuel Eto’o kughairi kustaafu na Wikiendi hii atakuwa huko Rades Nchini Tunisia kuiongoza Cameroun itakapocheza na Tunisia.
Asamoah Gyan atakuwa na Nchi yake Ghana watakapoikaribisha Egypt huko Kumasi na huko Addis Ababa, John Mikel Obi atakuwa na Nigeria itakayocheza na Ethiopia.
Nae Jonathan Pitroipa, ambae ndie aliteuliwa Mchezaji Bora AFCON 2013, atakuwa na Burkina Faso huko Ouagadougou kucheza na Algeria.

KOMBE LA DUNIA 2014
AFRIKA
Raundi ya Mwisho ya Mtoano
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Mechi za Kwanza:
Jumamosi Oktoba 12
19:00 Burkina Faso v Algeria
20:00 Ivory Coast v Senegal
Jumapili Oktoba 13
16:00 Ethiopia v Nigeria
20:00 Tunisia v Cameroon
Jumanne Oktoba 15
19:00 Ghana v Egypt
Marudiano:
Jumamosi Novemba 16
18:00 Nigeria v Ethiopia
22:00 Senegal v Ivory Coast
Jumapili Novemba 17
17:30 Cameroon v Tunisia
Jumanne Novemba 19
19:00 Egypt v Ghana
21:15 Algeria v Burkina Faso
**FAHAMU: Washindi 5 ndio watacheza Fainali za Kombe la Dunia

Kwenye Fainali za Kombe la Dunia zilizopita ambazo zilichezwa Afrika Kusini Mwaka 2010, Algeria, Cameroon, Ghana, Ivory Coast na Nigeria ndizo ziliiwakilisha Afrika, paamoja Wenyeji Afrika Kusini, na safari hii pia Nchi hizo, ukuiondoa Afrika Kusini, zina nafasi kwenda Brazil.
Kocha wa Ivory Coast, Sabri Lamouchi, amemwita Sentahafu wa Liverpool, Kolo Toure, ili kuungana na Kaka yake Yaya Toure kuhakikisha wanaifunga Senegal Mjini Abidjan.
Senegal wamemwacha Demba Ba kwa vile hachezi mara kwa mara Klabuni kwake Chelsea na badala yake kumtegemea Papiss Cisse wa Newcastle.
Similar Videos