Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

JOSÉ MOURINHO: ‘KUFURAHISHA WACHEZAJI SI TATIZO LANGU!’

Views:
Video Information


MOURINHO-CHELSEA_TRAININGMeneja wa Chelsea, José Mourinho, alipohojiwa ni jinsi gani atakimudu Kikosi chake kikubwa chenye Wachezaji wengi na kila mmoja kumfanya awe na furaha kwa kumpa Namba kila Mechi, alijibu kwa mkato kuwa hilo si tatizo lake na ni juu ya Wachezaji wenyewe kung’ara Uwanjani.
Alhamisi mara baada ya Wachezaji kurudi Klabuni kwao baada ya kuwa kwenye Mechi za Kimataifa na Nchi zao, Mourinho alikikusanya Kikosi chake chote pamoja na Wachezaji wapya, Straika Samuel Eto'o na Kiungo Willian, na kuwapa dibaji fupi ili kuwaweka sawa.
Lakini tayari kuna minong’ono kuhusu Mourinho ya kutowachezesha baadhi ya Wachezaji na Juan Mata ni mmoja wao ambae amecheza Dakika 65 tu kwenye Msimu huu licha ya kuwa mmoja wa Mastaa waliong’ara Msimu uliopita.
Lakini Mourinho amejibu: “Sijui kama ninaweza kuwafanya wawe na furaha au hapana. Lakini mimi nina furaha kwa sababu nina Wachezaji wengi wazuri na kama nafanya vizuri au vibaya, nafanya kwa nia njema tu. Waache wazungumze Uwanjani. Nitaamua ya Uwanjani tu na si Hadhi, Maneno, Mahojiano, Mawakala, Wazazi au Marafiki, si Magazetini au Twitter au lolote. Nitaacha Mpira uzungumze! Na Mpira utaamua!”
Alipohojiwa na Mwanahabari kutoka Belgium kama Kevin De Bruyne atachezeshwa Mechi 20 Msimu huu, Mourinho alijibu kwa mkato: “Kama hachezi Mechi 20 ni kwamba hastahili kucheza. Kama anastahili atacheza tu!”
Kuhusu Mata, Mourinho alifafanua kuwa Mchezaji huyo hatengwi na atapata Nafasi za kucheza kwani zipo Mechi nyingi zinazokuja mfululizo.
WENGER AMTETEA JACK WILSHERE NAADA KUPONDWA ENGLAND
Arsène Wenger amemtetea Kiungo wake Jack Wilshere kwamba atakuwa nguzo ya Timu ya TaifaWILSHERE_NA_UKRAINE ya England.
Wilshere alipondwa na Wadau wa England baada ya kucheza ovyo katika Mechi ya Ukraine na England iliyochezwa Jumanne iliyopita.
Wenger amedai Wilshere hayuko fiti kwa Asilimia 100 na hilo linamfanya kipaji chake kisionekana.
Wenger amesema: ”Akiendelea kucheza Mwezi Oktoba na Novemba basi hali yake itarudi kawaida.”
Pia, Wenger alafafanua kuwa Wachezaji mara nyingi wanashindwa kuonyesha cheche zao wakiwa na Timu za Taifa kwa sababu ya presha na matarajio makubwa ya Washabiki na Nchi zao.
Wenger alisema: “Wilshere akicheza Arsenal chini ya kiwango tunamwelewa na kukubali ni leo tu. Lakini kwenye Timu ya Taifa hilo likitokea kila Mtu anahoji uwezo wake. Mchezaji anapata shida na presha hiyo. Timu za Taifa zinahitaji Mastaa wanaoweza kuhimili presha hizo. France tulikuwa nae Zidane. Kabla alikuwepo Platini. Katika historia ya France, matokeo yalisimama pale Platini alipoacha kucheza. Yalisimama Zidane alipoacha. Unahitaji Kizazi kizuri cha Wachezaji lakini unahitaji Mchezaji spesho!”
Wenger anaamini Wilshere anaweza kuwa Mchezaji huyo Spesho kwa England.
DAVID MOYES ATETEA KUTOMCHEZESHA SHINJI KAGAWA
MOYES_NA_WASAIDIZIDavid Moyes amesema sababu kubwa ya baadhi ya Wachezaji wake kutocheza Mechi nyingi Msimu huu ni kwa sababu ya majukumu yao na Timu zao za Taifa.
Mmoja wa Wachezaji hao ni Mchezaji wa Japan Shinji Kagawa ambae Msimu huu amecheza Dakika 7 tu akitokea Benchi.
Lakini Bosi huyo wa Mabingwa Manchester United amesema ni kwamba Kagawa alichelewa kujiunga na wenzake kwa ajili ya Mazoezi ya kujitayarisha kwa Msimu mpya kwa vile alikuwa na Timu ya Taifa ya Japan huko Brazil kucheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara na pia aliporudi Manchester alilazimika kupiga tripu mbili za kwenda Japan kuichezea Nchi yake Mechi mbili huku kwao.
David Moyes amesema: “Kutocheza kwao ni kwa sababu ya kutokuwepo kwao.”
Vile vile, Moyes alifafanua kuwa walitaka kumnunua Fulbeki wa kushoto wa Everton Leighton Baines si kwa sababu ya kumwondoa Patrice Evra.
Alisema: “Tulihitaji Mtu wa kumsaidia. Msimu una Mechi 60 au 70 na akikosekana Patrice kucheza lazima awepo Mtu. Ukiichezea Man United Siku zote yupo Mtu anaejitayarisha kuichukua Jezi yako! Ni juu yako kupigana na kubaki nayo!”
Similar Videos