Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

JORGE MENDES: ‘RONALDO NI BORA KULIKO MESSI, NEYMAR!!’

Views:
Video Information


RONALDO-AUG13SUPASTAA wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ni Mchezaji Bora zaidi ya Wachezaji Mastaa wa Barcelona, Lionel Messi na Neymar, ingawa Barcelona ndio Klabu Bora katika historia.
Msimamo huo ni wa Jorge Mendes ambae ni Wakala wa Supastaa Cristiano Ronaldo ambae pia Wateja wake wengine ni pamoja na Jose Mourinho na Radamel Falcao.
Jorge Mendes vile vile amedai Ronaldo ni Mchezaji aliekamilika kila idara kuliko Lionel Messi.
Hapo Jana, Ronaldo, mwenye Miaka 28, alisaini Mkataba mpya utakaomweka huko Real Madrid kwa Miaka mitano zaidi na kumfanya awe ndie Mchezaji anaelipwa juu zaidi kupita yeyote Duniani.
Akisisitiza kuwa Ronaldo ni Bora kuliko Muargentina Messi, ambae ametwaa FIFA  Ballons d'Or mara 4, na Mbrazil Neymar, aliejiunga Barca hivi karibuni, Mendes alitamka: “Bila ya kuwakwaza Messi na Neymar, ukweli ni kuwa Ronaldo ni bora yao na ni Mchezaji aliekamilika. Lazima umsifie Mchezaji ambae, katika Miaka mine iliyopita, amefunga Bao katika kila Mechi ya Real Madrid aliyocheza!”
Katika Mechi 203 Ronaldo alizoichezea Real Madrid tangu ahamie hapo Mwaka 2009 kutoka Manchester United amefunga Mabao 203.
Hata hivyo Mendes alikiri kuwa Barcelona ndio Timu Bora Duniani pale aliposema: “Barcelona ndio Timu Bora katika historian na ni msingi wa Timu ya Taifa ya Spain! Wachezaji wao wana nafasi kubwa ya kufunga. Cristiano anachezea Timu ambayo akiwepo inang’ara asipokuwepo Timu imefifia! Ni ngumu kwake!”
Similar Videos