Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

Jakamoyo la Ufaransa kuhusu matokeo ya mashambulio ya kijeshi Mali

Views:
Video Information

Mashambulio ya anga ya jeshi la Ufaransa katika ngome za waasi kaskazini mwa Mali licha ya kuwa, mwanzoni yalishabikiwa na viongozi wa Paris, lakini habari zinazoripotiwa hivi sasa zinaonyesha kuwa, viongozi wa Ikulu ya Elysee wameingiwa na kihoro kutokana na tishio la kulipiza kisasi lililotolewa na al-Qaeda na wanamgambo wanaofungamana na mtandao huo. Rais Francois Hollande wa Ufaransa amesema kuwa, serikali yake imechukua hatua za kuimarisha usalama katika maeneo ya watu wengi ikihofia mashambulio ya kulipiza kisasi kutokana na kuingia kijeshi kaskazini mwa Mali. Kwa hakika wasiwasi wa Rais Hollande sio wa bure; kwani mmoja wa wasemaji wa al-Qaeda kaskazini mwa Afrika ametoa indhari kwa Ufaransa na kuitaka itazame upya uamuzi wake wa kushiriki katika operesheni ya kijeshi dhidi ya waasi wa Mali. Abou Dardar  mmoja wa viongozi waandamizi wa Harakati ya Tawhidi na Jihadi Magharibi mwa Afrika (MUJAO) ameitahadharisha Ufaransa na kusema kuwa, ijiandae kukabiliwa na mashambulio ya kulipiza kisasi ya wapiganaji wao. Hata Manuel Valls, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa amesisitiza kwamba, hali ya sasa nchini Mali inaweza kuandaa uwanja wa raia wa Ufaransa na maslahi ya Paris kuhujumiwa. Licha ya kuweko vitisho hivyo na manung'uniko ya wananchi pamoja na vyama vya kisiasa vya Ufaransa dhidi ya hatua ya Paris ya kuingia kijeshi nchini Mali, lakini Rais Francois Hollande ametia pamba masikioni na kutangaza wazi kuunga mkono kutumwa majeshi ya nchi hiyo kaskazini mwa Mali. Hatua ya Ufaransa ya kuingia kijeshi inaonekana haijapata himaya ya kila upande barani Ulaya. Msemaji wa Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, umoja huo hauna nia ya kuingia kijeshi huko Mali bali utatuma tu wanajeshi wa kutoa mafunzo kwa vikosi vya Bamako. Mjumbe na mwakilishi wa Russia katika masuala ya Afrika ametangaza kuwa, operesheni yoyote ile ya kijeshi dhidi ya wanamgambo wa Mali inapaswa kuidhinishwa na kupasisha na Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa. Ndani ya Ufaransa mambo si shwari kwani sauti za ukosoaji hatua ya jeshi la nchi hiyo kuingia kijeshi huko Mali zinazidi kuongeza. Viongozi wa chama cha mrengo wa kulia nchini humo wanasema kuwa, Rais Hollande amefanya kosa kuingia kijeshi huko Mali bila ya kushauriana na Bunge pamoja na Baraza la Mawaziri. Dominique de Villepin, Waziri Mkuu wa zamani wa Ufaransa naye amejitokeza na kuikosoa hatua hiyo ya Rais Holllande na kusisitiza kwamba, haikuwa sahihi. Kukithiri malalamiko na ukosoaji huo kumewafanya Waziri wa Mashauri ya Kigeni  na Waziri wa Ulinzi Laurent Fabius na Jean- Yves le Drian kwenda katika kikao cha baraza la taifa la nchi hiyo, kilichoitishwa kwa lengo la kujadili uingiaji kijeshi wa Paris huko Mali na uhalali wa hatua hiyo. Licha ya kuwa viongozi wa Ufaransa wanadai hatua yao hiyo ni ya kibinadamu yenye lengo la kuunga mkono mamlaka ya kujitawala Mali, lakini weledi wa mambo wanaamini kwamba, lengo kuu la Paris kuingia kijeshi katika nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika ni kudhibiti vyanzo vya utajiri vya nchi hiyo.
Similar Videos