Matangazo

ZILIZO KUPITA HIZI HAPA.

Bongo Flava ni sawa na mtoto anayelelewa na mama peke yake

Djokovic atwaa taji la Australian Open

Views:
Video Information
Novak Djokovic akishangilia ubingwa wa Australian Open
Katika mashindano ya Tennis mchezaji nambari moja duniani Novak Djokovic, leo ameshinda taji la la nne katika mashindano ya tennis ya Australia Open pale alipomuangusha Andy Murray, katika fainali.
Mchezaji huyo kutoka Serbia, alitumia muda wa saa tatu na dakika arobaini kumshinda Murray kwa seti tatu kwa moja za 6-7 7-6 6-3 na 6-2.
Andy Murray akiokoa moja ya mipira
Hata hivyo juhudi za Murray za kushinda kombe hilo mwaka huu, ziliingia kasoro baada ya kupata jeraha la mguu, ambalo lilimfanya kushindwa kukabiliana na mpinzani wake.
Kufuatia ushindi huo, Djokovic sasa ameshinda mataji sita katika mashindano ya tennis ya Grand slam na kuandikisha historia ya kuwa mtu wa kwanza kuwahi kushinda fainali za mashindano hayo ya Australia kwa miaka mitatu mfululizo, tangu miaka arobaini na sita iliyopita.
Similar Videos